Ridhiwani Kikwete aanza kupiga hesabu za bungeni

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM, Ridhiwani Kikwete.
Bagamoyo. Mgombea Ubunge wa Jimbo la 
Chalinze kwa tiketi ya CCM, Ridhiwani Kikwete ameanza kujinadi akisema 
endapo ataingia bungeni, atawaelimisha wabunge juu ya kuweka mbele 
maslahi ya Watanzania badala ya kulalamikia posho.
Ridhiwani ambaye juzi alithibitishwa 
na Kamati Kuu ya CCM kuwa mgombea wa jimbo hilo lililowahi kuongozwa na 
baba yake, Jakaya Kikwete alisema kitendo cha kutumia muda mwingi 
kubishania kanuni na wengine kulalamikia posho kinatia aibu kwani 
Watanzania wanahitaji Katiba Mpya.
Alisema hayo jana alipozungumza na 
waandishi wa habari baada ya kuchukua fomu ya kuwania ubunge wa jimbo 
hilo katika Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo.
Ridhiwani alisema, ikiwa atapata fursa
 ya kuingia bungeni, atawaelimisha wabunge wa Katiba ili waweze 
kuangalia maslahi ya wananchi kwanza na si kugombea posho.
Alisema, kitendo kinachotokea kwenye 
Bunge Maalumu la Katiba cha wajumbe kugombea posho kinatia aibu, hivyo 
basi wanapaswa kuelimishwa, ili waweze kujua wajibu wao.
Ridhiwani alisema kinachoonekana katika Bunge hilo ni kutunishiana misuli na si kuangalia maslahi ya wananchi,
Kutokana na hali hiyo, alisema wajumbe hao wanapaswa kuwa na moyo wa uzalendo na kuangalia maslahi ya wananchi.
waliowawakisliha pale, na si kuangalia mambo yao binafsi, jambo ambalo linaweza kuongeza migogoro.
Chanzo, mwananchi (R.M)
No comments:
Post a Comment