TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, March 10, 2014

Ridhiwani Kikwete aanza kupiga hesabu za bungeni 

ridhiwan_863e5.png
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM, Ridhiwani Kikwete.
Bagamoyo. Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM, Ridhiwani Kikwete ameanza kujinadi akisema endapo ataingia bungeni, atawaelimisha wabunge juu ya kuweka mbele maslahi ya Watanzania badala ya kulalamikia posho.
Ridhiwani ambaye juzi alithibitishwa na Kamati Kuu ya CCM kuwa mgombea wa jimbo hilo lililowahi kuongozwa na baba yake, Jakaya Kikwete alisema kitendo cha kutumia muda mwingi kubishania kanuni na wengine kulalamikia posho kinatia aibu kwani Watanzania wanahitaji Katiba Mpya.
Alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari baada ya kuchukua fomu ya kuwania ubunge wa jimbo hilo katika Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo.
Ridhiwani alisema, ikiwa atapata fursa ya kuingia bungeni, atawaelimisha wabunge wa Katiba ili waweze kuangalia maslahi ya wananchi kwanza na si kugombea posho.
Alisema, kitendo kinachotokea kwenye Bunge Maalumu la Katiba cha wajumbe kugombea posho kinatia aibu, hivyo basi wanapaswa kuelimishwa, ili waweze kujua wajibu wao.
Ridhiwani alisema kinachoonekana katika Bunge hilo ni kutunishiana misuli na si kuangalia maslahi ya wananchi,
Kutokana na hali hiyo, alisema wajumbe hao wanapaswa kuwa na moyo wa uzalendo na kuangalia maslahi ya wananchi.
waliowawakisliha pale, na si kuangalia mambo yao binafsi, jambo ambalo linaweza kuongeza migogoro.
Chanzo, mwananchi (R.M)

No comments:

Post a Comment