CRIMEA YATANGAZA RASMI KUWA SEHEMU YA SHIRIKISHO LA RUSSIA

Wanawake wa Crimea wakiwa Simferopol, Ukraine wakifurahia kujitenga kwao kutoka Ukraine na kuwa sehemu ya Russia
Maafisa katika Jamhuri ya Crimea 
iliyojitenga na Ukraine wanasema wapiga kura kwa idadi kubwa 
wameidhinisha kujiunga na Russia katika kura ya maoni iliyokuwa na utata
 ambayo imefanya viongozi wa magharibi kujiandaa na vikwazo dhidi ya 
Moscow. Jumatatu bunge la Crimea liliidhinisha kura ya maoni, kutangaza 
uhuru na kuwa rasmi sehemu ya Russia.
Hivi sasa imetangazwa rasmi wa-Crimea 
tayari wapo chini ya udhibiti wa Russia na wanaiunga mkono Russia 
wamefanya uchaguzi wa kujitenga kutoka Ukraine na kuungana na Russia. 
Kufuatia kura ya jumapili ya kujiunga na Russia, bunge la kieneo la 
Crimea limeomba kuwa sehemu ya shirikisho la Russia.
Lakini nini kinachofuata baada ya kura
 ya maoni, wote viongozi kwenye peninsula ya Black Sea na dunia 
waligawanyika katika njia ambazo zinakumbusha mivutano ya enzi ya vita 
baridi, viko mbali kumalizika.
Wabunge huko Moscow wanaahidi kuweka 
kando vikwazo vya kisheria ili kuiruhusu Crimea kuingia kwenye 
shirikisho la Russia. Lakini wasi wasi wa haraka kwa eneo ambalo halina 
mpaka wa ardhi na Russia unajumuisha usambazaji wake wa nishati, maji na
 bidhaa nyingine za msingi ambazo hivi sasa wanayapata kutoka Ukraine.
Moscow inatetea hatua ya Crimea kama 
kuongeza kanuni za kujitambua wenyewe. Mazungumzo kwa njia ya simu kati 
ya Rais wa Marekani Barack Obama na Rais wa Russia Vladimir Putin 
yanaripotiwa kuleta mafanikio kidogo kuziba mwanya uliopo.
Waangalizi wa kigeni walioalikwa na 
Crimea inayoungwa mkono na serikali ya Russia walitetea kura ya maoni 
kama inaendeleza kanuni za kimataifa. Mwangalizi kutoka Ubelgiji, Frank 
Creyelman aliwapuuza wakosoaji wakiwemo kutoka serikali mpya huko Kyiv 
kwamba upigaji kura ulifanyika kwa mtutu wa bunduki.
Chanzo, voaswahili (R.M)
No comments:
Post a Comment