TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, March 16, 2014



 JICA WAJIPANGA KUIPIGA TAFU TANZANIA KWA UJENZI WA DARAJA

SHIRIKA lisilo la kiserikali toka Nchini Japan , JICA ALUMNI ASSOCIATION OF TANZANIA (JATA)  imejipanga kwa mwaka huu kusimamia miradi mikubwa miwili kwa mwaka 2014/2015 itakayofadhiliwa na Serikali ya Japan  hapa nchini.
Miradi hiyo imetajwa kuwa ni ujenzi wa daraja la juu , litakalojengwa  eneo la Tazara  na maendeleo ya elimu  katika viwanda  na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.
Hayo yalisemwa na Mwakilishi Mkuu wa JICA Bw.  Yasunori Onishi , wakati akifungua mkutano wa mwaka wa  JATA , ambapo alisema kuwa kwa sasa Tanzania na Japani imejenga  mahusiano mazuri na raia wao wengi wapo nchini kwa ajili ya kufanya biashara  na kutekeleza miradi ya maendeleo.
Bw. Onishi alisema Serikali ya Japani inampango wa kutekeleza miradi hiyo mikubwa miwili ndani ya mwaka 2014/2015 kwa lengo la kuboresha mahusiano zaidi  juu ya kuwawezesha vijana wengi kupata elimu ya viwanda  ili wajijengee uwezo wa kujiajiri .
“ Mbali na hilo lazima tuwekeze pia kwenye miumdo mbinu kama kujenga hilo daraja la juu ambapo itasaidia kupunguza msongamano wa foleni za  magari ambapo kwa sasa ni kero kubwa jijini na daraja hilo litajengwa eneo la Tazara” alisema Bw. Onishi
Alisema mbali na miradi hiyo ambayo imepangwa kutekelezwa ,  Japani kwa  kupitia JICA imekwisha  tekeleza miradi mbali mbali nchini  kama kukabiliana na utatuzi wa tatizo la  maji na umeme  katika visiwa vya Unguja na Pemba , kusimamia maswala ya mazingira, kusimamia miradi mikubwa ya maji  katika mto wa Wami Dakawa.
Aliendelea kueleza kuwa mambo mengine waliyofanya ni  kuibua ushindani wa wanadunzi wa shule za sekondari katika kuandisha insha na kuwapatia zawadi , Kutembelea na kutoa ushauri  wa kitaalamu katika chuo cha teknolojia kilichopo Mkoani Kilimanjaro, Miradi ya kilimo cha umwagiliaji , mradi wa kutengeneza vyombo vya udongo , Pamoja na mradi wa ufuatiliaji wa mipango mikakati  katika maendeleo ya majimbo Zanzibar.
Hata hivyo Naibu Katibu Mkuu wa JATA  nchini Bw. Omar Kassim Omar alisema Serikali ya Japani kwa kupitia shirika lao hilo, imekuwa ikifadhili na kuendelea kufadhili  shughuli mbalimbali za maendeleo hapa nchini , ambapo wameona zikiwa katika mafanikio makubwa  hasa kwenye upande wa kutoa elimu kwa vijana, kwani wapo baadhi ya wajapani wamekuwa wakitoa mafunzo katika shule za sekondari ya sayansi na hisabati  bure.
Alisema JATA  imepanga kuibua miradi mbali mbali ikiwemo ya afya, mazingira, elimu, kuendesha semina kwa vijana  na mambo mengine ambazo zitasimamiwa vema na kufadhiliwa na Japan.
Mbali na hayo JATA pia ilifanya uchaguzi wa viongozi wapya watakao simamia vema utekelezaji wa miradi iliyopangwa kufanyika ambapo nafasi ya Mwenyekiti ilishikwa na Bw. Twaha  Twaha , Makamu Mwenyekiti ni Bw. Omar Kassim Omar,  Katibu ni Edna Ngeregeza  na katibu Msaidizi ni  Bw. Perer Mtaita na mweka hazina ni Zuhura Mwakijinja.
Wajumbe wengine wanaounda kamati ni  Kassimu Shaali , Jacob Kattanga, Milton Rwegasira na Mudrick Fadhili Abasi.

Mwisho

No comments:

Post a Comment