JICA WAJIPANGA KUIPIGA TAFU TANZANIA KWA UJENZI WA DARAJA
SHIRIKA lisilo la kiserikali toka Nchini Japan , JICA ALUMNI
ASSOCIATION OF TANZANIA (JATA) 
imejipanga kwa mwaka huu kusimamia miradi mikubwa miwili kwa mwaka
2014/2015 itakayofadhiliwa na Serikali ya Japan 
hapa nchini.
Miradi hiyo imetajwa kuwa ni ujenzi wa daraja la juu ,
litakalojengwa  eneo la Tazara  na maendeleo ya elimu  katika viwanda  na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.
Hayo yalisemwa na Mwakilishi Mkuu wa JICA Bw.  Yasunori Onishi , wakati akifungua mkutano wa
mwaka wa  JATA , ambapo alisema kuwa kwa
sasa Tanzania na Japani imejenga 
mahusiano mazuri na raia wao wengi wapo nchini kwa ajili ya kufanya
biashara  na kutekeleza miradi ya
maendeleo.
Bw. Onishi alisema Serikali ya Japani inampango wa
kutekeleza miradi hiyo mikubwa miwili ndani ya mwaka 2014/2015 kwa lengo la
kuboresha mahusiano zaidi  juu ya
kuwawezesha vijana wengi kupata elimu ya viwanda  ili wajijengee uwezo wa kujiajiri .
“ Mbali na hilo lazima tuwekeze pia kwenye miumdo mbinu kama
kujenga hilo daraja la juu ambapo itasaidia kupunguza msongamano wa foleni
za  magari ambapo kwa sasa ni kero kubwa
jijini na daraja hilo litajengwa eneo la Tazara” alisema Bw. Onishi 
Alisema mbali na miradi hiyo ambayo imepangwa kutekelezwa
,  Japani kwa  kupitia JICA imekwisha  tekeleza miradi mbali mbali nchini  kama kukabiliana na utatuzi wa tatizo la  maji na umeme 
katika visiwa vya Unguja na Pemba , kusimamia maswala ya mazingira,
kusimamia miradi mikubwa ya maji  katika
mto wa Wami Dakawa.
Aliendelea kueleza kuwa mambo mengine waliyofanya ni  kuibua ushindani wa wanadunzi wa shule za
sekondari katika kuandisha insha na kuwapatia zawadi , Kutembelea na kutoa
ushauri  wa kitaalamu katika chuo cha teknolojia
kilichopo Mkoani Kilimanjaro, Miradi ya kilimo cha umwagiliaji , mradi wa
kutengeneza vyombo vya udongo , Pamoja na mradi wa ufuatiliaji wa mipango
mikakati  katika maendeleo ya majimbo
Zanzibar.
Hata hivyo Naibu Katibu Mkuu wa JATA  nchini Bw. Omar Kassim Omar alisema Serikali
ya Japani kwa kupitia shirika lao hilo, imekuwa ikifadhili na kuendelea
kufadhili  shughuli mbalimbali za
maendeleo hapa nchini , ambapo wameona zikiwa katika mafanikio makubwa  hasa kwenye upande wa kutoa elimu kwa vijana,
kwani wapo baadhi ya wajapani wamekuwa wakitoa mafunzo katika shule za sekondari
ya sayansi na hisabati  bure.
Alisema JATA  imepanga
kuibua miradi mbali mbali ikiwemo ya afya, mazingira, elimu, kuendesha semina
kwa vijana  na mambo mengine ambazo
zitasimamiwa vema na kufadhiliwa na Japan.
Mbali na hayo JATA pia ilifanya uchaguzi wa viongozi wapya
watakao simamia vema utekelezaji wa miradi iliyopangwa kufanyika ambapo nafasi
ya Mwenyekiti ilishikwa na Bw. Twaha 
Twaha , Makamu Mwenyekiti ni Bw. Omar Kassim Omar,  Katibu ni Edna Ngeregeza  na katibu Msaidizi ni  Bw. Perer Mtaita na mweka hazina ni Zuhura
Mwakijinja.
Wajumbe wengine wanaounda kamati ni  Kassimu Shaali , Jacob Kattanga, Milton
Rwegasira na Mudrick Fadhili Abasi.
Mwisho
No comments:
Post a Comment