SERIKALI YAINGILIA KATI ADA YA VYUO VIKUU
Serikali imekunjua makucha yake katika kudhibiti ada zinazotozwa katika vyombo vya utoaji elimu chini.
Jana, 
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa alizindua 
rasmi mfumo mpya wa ulipaji ada katika vyuo vya elimu ya juu, huku 
akisema utasaidia kudhibiti viwango vya ada vinavyotozwa kwa wanafunzi.
Akizindua
 mfumo huo jijini Dar es Salaam, Dk. Kawambwa alisema Serikali 
imeanzisha mfumo huo unaotarajiwa kuanza kutumika mwaka huu katika vyuo 
vyote, kwa lengo la kudhibiti ada kulingana na fani zinazotolewa.
"Sasa 
natarajia nitapata usingizi wa kueleweka maana kelele za viwango vya ada
 zilikuwa ni kubwa, kila chuo kilikuwa na ada yake. Niliulizwa vigezo 
vinavyotumika kupanga sikuwa na jibu, lakini sasa nitakuwa na majibu 
tena yanayoeleweka," alisema.
Suala la 
viwango vya ada katika shule na vyuo binafsi liliwahi kuzungumziwa kwa 
kina siku za nyuma, huku Rais Jakaya Kikwete na Waziri Kawambwa 
wakinukuliwa kwa nyakati tofauti kutaka taasisi za elimu kupunguza 
viwango vya elimu. Aprili 2013 akifungua Mkutano Mkuu Maalumu wa Chama 
cha Wamiliki na Mameneja wa Shule na Vyuo Visivyokuwa vya Serikali 
(Tamongsco) uliofanyika mkoani Mbeya, Rais Kikwete alisema: "Elimu ni 
huduma muhimu na haki kwa mtoto. Siyo vyema kugeuzwa kuwa biashara ya 
kuleta faida kubwa.''
Aliongeza
 kuwa Serikali ilikuwa katika mchakato wa kutathmini ada zinazotozwa 
vyuoni na sekondari ili kupendekeza viwango halisi vinavyopaswa kutozwa.
Kwa sasa 
udadisi wa gazeti hili umebaini kuwa wanafunzi walioanza masomo katika 
mwaka wa fedha 2013/2014 wanatozwa ada kuanzia Sh360,000 kwa mwaka hadi 
Sh9,900,000.
Kwa 
mujibu wa Dk. Kawambwa, mfumo huu ambao baadaye utaendelea hadi shule za
 sekondari na msingi, umepatikana kupitia kikosi kazi cha wataalamu 
ambacho pamoja na majukumu mengine kilipewa kazi ya kutathmini gharama.
Dk. 
Kawambwa alisema moja ya faida ya utaratibu huo mpya ni kudhibiti 
taasisi zinazotoza ada kubwa kwa sababu za binafsi ikiwamo biashara.
Mkuu wa 
Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini Makumira cha Dar es Salaam (Tudarco), 
Profesa Uswege Minga alisema endapo gharama hizo zitakuwa sawa, vyuo 
binafsi vitaathirika kwa sababu ni gharama kubwa kuendesha chuo kikuu.(P.T)

No comments:
Post a Comment