MKUU WA JESHI KUGOMBEA URAIS MISRI

Mkuu wa 
majeshi na waziri wa ulinzi Misri, Abdul Fattah al-Sisi, ametangaza 
kujiuzulu jeshini ili kugombea katika uchaguzi wa urais mwezi ujao.
Wagombea wote wanapaswa kuwa raia.
Akizungumza
 Kwenye hotuba ya Televisheni huku akiwa amevalia sare ya kijeshi Abdel 
Fattah El Sissi amesema yeye sio mwanajeshi tena baada ya miaka 44 na 
kwamba amechukua hatua hiyo ili aweze kutimiza jukumu lingine muhimu.
Ni Bayana kwana Sisi hatakua na 
kibarua kigumu kujipatia ushindi katika uchaguzi wa Urais. Anaungwa 
mkono na idadi kubwa ya raia wa Misri na hadi sasa hana wapinzani 
wowote.
Baadhi ya waliotaka kugombea urais wamejiondoa wakidai kwamba hawataweza kuendesha kampeni zao kwa njia huru.
Wafuasi wake Sisi wanamuona kama 
kiongozi imara ambaye anaweza kurejesha amani na udhabiti nchini Misri 
baada ya miaka mingi ya machafuko.
Wakosoaji wake wanasema ana msimamo mkali na amechangia pakubwa katika kusambaratisha na kuhujumu upinzani nchini Misri.
Mkuu huyo wa jeshi atakabiliwa na 
majukumu mazito ya kufufua uchumi uliofifia , kupambana na uasi na 
kuileta pamoja nchi iliyogawanyika. Ameahidi kutekeleza mabadiliko 
makubwa lakini akaonya kuwa hawezi kufanya miujiza.
Chanzo:BBC
No comments:
Post a Comment