TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, March 9, 2014

MANCHESTER CITY YATUPWA NJE KOMBE LA FA 

wigan_9e6d5.jpg
wachezaji wa timu ya Wigani wakimpongeza Jodri Gomez baada ya kupachika goli kwa njia ya mkwaju wa penati.
Na Riziki Mashaka.
Timu ya Wigan imeichapa Man City magoli 2-1 katika mchezo uliopigwa kwenye dimba la Etihad katika hatua ya robo fainali ya kombe la FA.
Jodri Gomez aliindikia Wigan goli la kwanza kwa mkwaju wa penati mnamo dakika ya 27, wakati James Perch alipachika goli la pili katika dakika ya 34 na kuiwezesha timu hiyo kuibuka na ushindi wa magoli 2-0 mpaka timu hizo zikienda mapumziko, Samir Nasri alipiga msumari wa moto na kumwacha mlinda mlango wa Wigan akishangaa na kuiwezesha timu hiyo kulipa goli 1 lakini mpaka mwisho wa mchezo, Man City ilijikuta ikiondolewa katika mtanange huonkwa jumla ya magoli 2-1.
Matokeo ya mchezo huo yameifanya timu ya Man City kutolewa katika kinyang'anyiro cha kombe hilo, itakumbukwa kuwa Man City walitolewa na Wigan katika fainali za kombe la FA mwaka jana, hivyo kichapo cha leo ni pigo jingine kwa timu hiyo ambayo siku chache zijazo itakumbana na Barcelona katika mchezo wa raundi ya pili ya kombe la klabu bingwa ya ulaya.

No comments:

Post a Comment