MAANDAMANO YASHTADI UKRAINE KUIPINGA SERIKALI HIYO

Miji ya 
kusini na mashariki nchini Ukraine imekuwa uwanja wa maandamano makubwa 
ya wananchi dhidi ya viongozi wa serikali ya nchi hiyo. Maelfu ya 
wananchi katika miji ya Donetsk, Kharkiv, Odessa na miji mingine ya 
kusini na mashariki mwa nchi hiyo, walimiminika mabarabarani hapo jana 
wakipinga mwenendo wa viongozi wa serikali ya Kiev. Kwa mujibu wa 
ripoti, waandamanaji wametaka nao kuitishwa kura ya maoni kwa ajili ya 
kujitenga na kujiunga na shirikisho la Russia kama lilivyofanya hivi 
karibuni jimbo la Crimea sanjari na kurejeshwa madarakani Viktor 
Yanukovych kama Rais wa halali aliyechaguliwa na wananchi wa nchi hiyo. 
Kwa upande mwingine, maelfu ya wananchi wamejitokeza mjini Kiev, mji 
mkuu wa Ukraine wakiunga mkono viongozi wa sasa na kutaka kudumishwa 
umoja wa kitaifa nchini humo. Hayo yanajiri katika hali ambayo suala la 
kujitenga eneo la Crimea kutoka Ukraine na kujiunga na Russia 
limeendelea kushadidisha uadui kati ya Moscow na nchi za Magharibi.
(J.G)
No comments:
Post a Comment