TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, March 24, 2014

MAANDAMANO YASHTADI UKRAINE KUIPINGA SERIKALI HIYO

40432AB7-5CDC-4B69-B647-CB503D486891_mw1024_n_s_d2bcc.jpg
Miji ya kusini na mashariki nchini Ukraine imekuwa uwanja wa maandamano makubwa ya wananchi dhidi ya viongozi wa serikali ya nchi hiyo. Maelfu ya wananchi katika miji ya Donetsk, Kharkiv, Odessa na miji mingine ya kusini na mashariki mwa nchi hiyo, walimiminika mabarabarani hapo jana wakipinga mwenendo wa viongozi wa serikali ya Kiev. Kwa mujibu wa ripoti, waandamanaji wametaka nao kuitishwa kura ya maoni kwa ajili ya kujitenga na kujiunga na shirikisho la Russia kama lilivyofanya hivi karibuni jimbo la Crimea sanjari na kurejeshwa madarakani Viktor Yanukovych kama Rais wa halali aliyechaguliwa na wananchi wa nchi hiyo. Kwa upande mwingine, maelfu ya wananchi wamejitokeza mjini Kiev, mji mkuu wa Ukraine wakiunga mkono viongozi wa sasa na kutaka kudumishwa umoja wa kitaifa nchini humo. Hayo yanajiri katika hali ambayo suala la kujitenga eneo la Crimea kutoka Ukraine na kujiunga na Russia limeendelea kushadidisha uadui kati ya Moscow na nchi za Magharibi.
(J.G)

No comments:

Post a Comment