KATIBU MKUU WA UMOJA WA MATAIFA AELEKEA  MOSCOW NA KYIEV
Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-moon.
Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki
 Moon yuko njiani kuelekea Moscow na Kyiev katika juhudi za kusaidia 
kutafuta suluhu la kidiplomasia kwa mzozo wa Peninsula ya Crimea.
Ofisi ya Bw.Ban imeeleza kwamba 
atawasili katika mji mkuu wa Russia Alhamisi na kukutana na rais Vladmir
 Putin. Na Pia atafanya mazungumzo na waziri wa mambo ya nje Sergei 
Lavrov na maafisa wengine wa juu .
Ijumaa ataelekea Ukraine ambako 
atakutana na rais wa mpito Oleksandr Turchymov na waziri mkuu wa muda 
Arseniy Yatsenyuk na pia maafisa wengine waandamizi.
Msemaji wa Umoja wa mataifa Farhan Haq
 alirudia kueleza kwamba katibu mkuu alikuwa akitarajia kupatikana 
suluhisho la kidiplomasia kwa suala hilo.
Siku ya Jumapili eneo la Crimea la 
Ukraine lilifanya kura ya maoni ya haraka kukiwepo maelfu ya wanajeshi 
wa Russia na kupiga kura ya kujitenga na Ukraine wakiwa na nia ya 
kujiunga na muungano wa Russia.Viongozi wa muda wa Ukraine wametangaza 
kura hiyo ni kinyume cha sheria chini ya katiba ya nchi hiyo.
Wakati wa ziara yake fupi katibu mkuu 
pia atakutana na wanachama wa tume ya wafuatiliaji wa umoja wa mataifa 
wakati akiwa Kyiv. Umoja wa mataifa umeomba kupeleka wasimamizi huko 
Crimea ili kutathmini hali ilivyo.
Chanzo, voaswahili (R.M)
No comments:
Post a Comment