TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, March 13, 2014

Inavyoendelea hali ya kiafya ya Michel Schumacher baada ya ajali mbaya

 Michael-Schumacher-slider-2971673Bingwa wa zamani wa mashindano ya Fomula 1 Michael Schumacher, amekuwa akionyesha dalili nzuri baada ya madaktari kuanza kumtoa katika hali yake mahututi.

Familia yake imesema kuwa bado ina matumaini kwamba Michael ataweza kuamka.
Madaktari nchini Ufaransa wamekuwa wakifanya juhudi za kumuamsha Michael ambaye ni bingwa mara saba wa Formula 1 kutoka katika hali yake ya kupoteza fahamu.
Schumacher mwenye umri wa miaka 45 kutoka Ujerumani, alipata majeraha mabaya ya kichwa alipokuwa anashiriki mchezo wa kuteleza kwa barafu mwezi Disemba 29 katika maeneo ya Alps Ufaransa.
Madaktari walimuweka Schumacher katika hali ya kupoteza fahamu ili kuzuia uvimbe katika ubongo wake.
Familia ya Schumacher imezungumza na kusifu jitihada za madaktari wa Ufaransa na pia wamesema kuwa hiki ni kipindi kigumu kwao na kuwa hawana budi ila kuwa na subira.
Wachunguzi wanasema kuwa Schumacher hakuwa anaenda kwa kasi kubwa wakati wa ajali hiyo ingawa alianguka alipokuwa akiteleza.
Schumacher alistaafu kutoka katika mashindano ya Formula 1 mwaka 2012 baada ya kushiriki mwa miaka 19.
Alishinda mataji mawili akiwa na kampuni ya Benetton mwaka 1994 na 1995,kabla ya kuhamia kampuni ya Ferrari mwaka 1996 na kuendelea kushinda mataji mengine matano kuanzia mwaka 2000.

No comments:

Post a Comment