TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, April 8, 2014

Uchaguzi mkubwa zaidi waanza India 


Shughuli ya kupiga kura inaendelea nchini India, taifa lililo kubwa zaidi duniani linaloongozwa kidemokrasia.
Watu milioni 814 watachagua kati ya chama kinachotawala cha Congress na chama cha Upinzani cha Hindu nationalist BJP .
Uchaguzi huu utaandaliwa katika mikondo 9 zikianzia majimbo ya Assam na Tripura zilizoko Kaskazini Mashariki mwa taifa hilo kubwa.
Shughuli hiyo kubwa zaidi ya Kidemokrasia duniani itachukua majuma matano kukamilika kutokana na changamoto ya maswala ya mipango usalama na idadi .
Chama kinachotawala cha Congress kinakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa chama cha mrengo wa kulia cha Hindu BJP, kinachoongozwa na Narendra Hodi, kiongozi mbishi mwenye ushawishi mkubwa kutoka Magharibi mwa Gujerati.
Kampeni za uchaguzi huo zimetawaliwa na maswala ya ufisadi pamoja na mfumuko wa bei ya bidhaa za Chakula.
Aidha Kuna Chama mahsusi ya Kupambana na Ufisadi yaani AAP (Anti-corruption party).
Chama hicho kipya kiliwaduwaza wachanganuzi wa maswala ya kisiasa nchini humo kilipotwaa ushindi muhimu katika Uchaguzi mdogo uliofanyika mji mkuu wa India New Delhi mwaka uliopita.
Chama hicho sasa kimewakilisha wagombea katika maeneo bunge yote 543
Bunge la chini la kitaifa ( Lok Sabha) linawajumbe 543 na chama chochote kinahitaji ushindi wa wajumbe 272 kuunda serikali mpya .
Idadi ya wapiga kura ni milioni 814 zaidi ya wapiga kura milioni 100 million zaidi ya wale waliopiga kura katika uchaguzi uliopita wa mwaka wa 2009.
Kutakuwa na vituo 930,000 takriban vituo laki moja zaidi ya vituo vilivyotumika mwaka wa 2009.
Mashini za kielektroniki za kupigia kura zitatumika na kwa mara ya kwanza hazitajumuisha kidude cha kutowachagua wawakilishi waliosajiliwa yaani None of the Above (Nota).
Mwandishi wa BBC aliyeko katika jimbo la Assam, Sanjoy Majumderameripoti kuwa wapiga kura walijitokeza kwa wingi asubuhi na mapema wakiwa wamevalia mavazi ya kitamaduni ya Sari huku wakiwa wamejitanda mitandio ya Kiassamese.
Wagombea wakuu ni mwakilishi wa familia ya Nehru-Gandhi, Rahul Gandhi wa chama cha Congress ambaye atakuwa akipambana dhidi ya Narendra Modi wa chama kikubwa cha upinzani BJP.
(MM)

No comments:

Post a Comment