TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, April 27, 2014

KAMATI YA MAADILI NA HAKI YAKWAMA KUMUHUKUMU WENJE

WENJE 7c351
Na Hudugu Ng'amilo
Hukumu dhidi ya mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Ezekiah Wenje imekwama kutolewa jana baada ya mjumbe huyo kushindwa kupatikana ili kuwasilisha utetezi wake.
Wenje anadaiwa kuwatuhumu mawaziri wanne akiwemo Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa kutoa rushwa kwa wajumbe wa kundi la 201, ili wapitishe kura ya wazi na kuunga mkono serikali mbili.
Viongozi wengine waliohusishwa na tuhuma hizo ni Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka.
Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samwel Sitta aliamua kulipeleka shauri kwenye kamati ya maadili na haki za Bunge, baada ya Wenje kukataa kufuta kauli yake na kuwaomba radhi wajumbe hao.
Akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo bungeni jana kwa niaba ya mwenyekiti, Pandu Ameir Kificho, makamu mwenyekiti, Dk Susan Kolimba alisema jitihada za kumtafuta Wenje bado zinaendelea.
Hata hivyo Dk Kolimba alisema kamati yake imefanikiwa kuwahoji Dk Kawambwa na Kabaka pamoja na wajumbe wawili kutoka kundi la 201 waliolalamika, Esther Mlimba na Dk Eve Semakafu.
"Mwenyekiti alipomtaka kuomba radhi alisema anaweza kuomba radhi kwa msingi tu kwamba ukweli aliousema umewaudhi watu, hivyo anaomba radhi kwa ukweli aliousema," alisema Dk Kolimba.
Alisema baada ya Wenje kutopatikana, kamati hiyo iliona ni busara kuwasikiliza mawaziri waliotuhumiwa pamoja na wale waliolalamikia kauli hiyo ya Wenje ambao ni Semakafu na Mlimba.
"Jitihada za kumtafuta Maghembe zilishindikana...Tunatarajia baada ya Wenje kufika mbele ya kamati tutawasilisha mapendekezo yetu mbele ya Bunge hili,"alisema Dk Kolimba.
Baada ya kutolewa kwa taarifa hiyo, Sitta alisema suala hilo litaamuliwa hapo baadaye baada ya kamati hiyo kukamilisha kazi yake ikiwamo kumhoji Wenje na wengine waliotuhumiwa.
:Chanzo Mwananchi.

No comments:

Post a Comment