Kura aina ya Muungano Agosti
Upigaji 
kura kupitisha sura mbili zinazohusu Muungano katika Bunge la Katiba 
umesogezwa mbele hadi Agosti litakapoitishwa tena, Mwananchi limebaini.
Vyanzo 
mbalimbali vimelidokeza gazeti hili jana kuwa upigaji kura hautafanyika 
sasa badala yake wajumbe wa Bunge wataendelea kuchangia hoja hadi Aprili
 28, mwaka huu wakati Bunge hilo litakapoahirishwa baada ya kukamilisha 
siku 70 za awali.
Awali, 
upigaji huo wa kura ambao umewagawa wajumbe katika makundi mawili; moja 
likitaka serikali tatu na jingine likitaka serikali mbili, ulitarajiwa 
kufanyika Ijumaa wiki hii ili kuhitimisha mvutano wa muda mrefu baina ya
 pande zinazopingana.
Chanzo 
chetu ndani ya Kamati ya Uongozi, kilidokeza jana kuwa hata baada ya 
Bunge hilo kurejea Agosti 5, mwaka huu, ikielezwa kuwa lengo ni kutoa 
fursa ya kuendelea kushawishi uungwaji mkono ili kupata theluthi mbili 
ya kura inayohitajika.(MM)
Mwenyekiti
 wa Bunge, Samuel Sitta alithibitisha kuahirishwa kwa upigaji wa kura 
huo, lakini akasema hiyo imetokana na wingi wa wajumbe wanaotaka 
kuchangia na si kitu kingine.
"Ni kweli
 wajumbe hawatapiga kura kwa sura mbili walizowasilisha hadi jana na 
lengo ni kuwapa nafasi wajumbe wengi zaidi kuchangia katika jambo hili 
zito," alisema Sitta.
Alisema 
hadi jana mchana alikuwa amepokea majina ya wachangiaji zaidi ya 400 
ambao wasingeweza kuchangia kwa siku tatu kama kanuni zinavyoelekeza.
Hata 
hivyo, alipotakiwa kutoa ufafanuzi zaidi juu ya jambo hilo alisema 
walikuwa wakutane kwenye kikao cha Kamati ya Uongozi kujadili pamoja na 
mambo mengine, suala hilo...
"Kwanza nisiseme sana, maana ndiyo tunaingia kwenye Kamati ya Uongozi, nitafuteni baada ya kikao nitawaelezeni."
Katika 
kipindi cha asubuhi, Sitta alisikika akiwataka wajumbe watoe hofu kuhusu
 dukuduku la Muungano kwa kuwa watapata fursa ya kuchangia mjadala kwa 
wiki nzima bila kufafanua kama itabidi kanuni itenguliwe au la.
Kwa 
mujibu wa Kanuni ya 33(7) ya Kanuni za Bunge Maalumu la Katiba za mwaka 
2014, baada ya taarifa za kamati hizo kuwasilishwa, zitajadiliwa katika 
kipindi kisichozidi siku tatu.
Sitta 
katika kipindi hicho cha asubuhi, alisema kila siku watachangia wajumbe 
50 na kila mmoja atatumia dakika 10 na kwa kuanzia, hiyo jana wajumbe 25
 walitarajiwa kupata fursa ya kuchangia.
CHANZO:MWANANCHI
No comments:
Post a Comment