Serikali yajitetea ubovu miundombinu

Wananchi 
wakipita kwa taabu katika sehemu finyu ya barabara ya Kilwa maeneo ya 
Mbagala, iliyoharibiwa na maji ya mvua na kusababisha magari kushindwa 
kupita. Picha na Venance Nestory
Dar es 
Salaam. Wizara ya Ujenzi imesema kuwa asilimia kubwa ya miundombinu 
iliyoharibiwa na mafuriko haikujengwa chini ya kiwango kama inavyodaiwa,
 bali ni matokeo ya uharibifu wa mazingira.(MM)
            
Akizungumza na gazeti hili jana, 
Msemaji wa wizara hiyo, Martin Ntemo alisema madaraja mengi 
yaliyoharibiwa na mvua zinazoendelea nchini yameliwa katika makutano na 
barabara na si kumeguka.
"Mito mingi imechepuka katika mikondo yake ya zamani kutokana na uharibifu wa mazingira unaofanywa na wakazi wa maeneo hayo kila kukicha.," alisema na kuongeza:
"Mito mingi imechepuka katika mikondo yake ya zamani kutokana na uharibifu wa mazingira unaofanywa na wakazi wa maeneo hayo kila kukicha.," alisema na kuongeza:
"Pia 
asilimia kubwa ya madaraja hayo yameshuka katika urefu wake wa awali 
kutokana na mchanga unaosababishwa na mmonyoko wa udongo, hivyo 
kupunguza sehemu iliyokuwa imekadiriwa kwa maji kupita."
Aliongeza
 kuwa madaraja na barabara hizo nyingi zilikuwa zimeshakabidhiwa muda 
mrefu kwa Serikali na kwamba Wizara inaendelea kutafuta suluhu ya 
kuyarudisha katika hali yake ya kawaida.
Mvua 
zinazoendelea kunyesha nchini zimeendelea kuharibu miundombinu 
mbalimbali ya barabara ambapo mawasiliano kati ya Jiji la Dar es Salaam 
na mikoani yalikatika kutokana na madaraja kuharibika na kufurika maji.
"Tulikuwa
 na wakati mgumu katika Daraja la Mpiji kutokana na uhaba wa mawe, 
lakini tayari tumeshapata sehemu ambayo malori yatakuwa yakichukua na 
kupeleka eneo la ujenzi," alisema Ntemo.
Alisema 
walifanikiwa kupata mawe eneo la Wazo Hill na viunga vyake ambayo 
yatasaidia kukamilisha ujenzi wa daraja hilo lililopo Barabara ya 
Bagamoyo kufikia leo asubuhi au mchana.
Kwa 
mujibu msemaji huyo, tayari Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na 
Kampuni za Ujenzi za Skol Building Contractors na Estim zinaendelea na 
ujenzi wa maeneo mbalimbali yaliyoathirika.
Alipoulizwa
 kuhusu gharama za jumla za uharibifu huo, alisema bado Wizara 
inaendelea kukusanya taarifa ikizingatiwa kwamba mvua bado zinaendelea 
kunyesha.
Aliongeza
 kuwa, Waziri aliagiza madaraja yote kutengenezwa usiku kucha 
kuhakikisha yanaendelea kuunganisha miji na mitaa kama awali.
"Wanajeshi
 wanaangalia jinsi ya kuweka daraja la dharura katika Daraja la Mto 
Kiziga ambalo kalavati liliharibika na pale Kongowe, daraja la Mto Kozi,
 wanajaza kifusi ili kufungua mawasiliano yaliyokuwa yamesitishwa," 
alisema.
CHANZO:MWANANCHI
No comments:
Post a Comment