MRIPUKO WAUWA 71 ABUJA

Hali ya taharuki kufuatia mripuko katika kituo cha basi katika kiunga cha Abuja,Nigeria. (14.04.2014)
Tuhuma 
zinaelekezwa dhidi ya kundi la Boko Haram juu ya kwamba hakuna taarifa 
ya kudai kuhusika na shambulio hilo kutoka kwa wapiganaji hao wa itikadi
 kali za Kiislamu ambapo hasa wamekuwa wakiendesha zaidi harakati zao 
kaskazini mashariki mwa Nigeria.Mbali ya watu 71 waliouwawa polisi 
imesema watu 124 wamejeruhiwa katika shambulio hilo ambalo ni la kwanza 
kufanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo katika kipindi cha miaka miwili.
Kamadori 
wa kikosi cha anga Charles Otengbade ambaye ni mkurugenzi wa oporesheni 
za msako na uokozi amesema wataalamu wa usalama wanashuku kwamba bomu 
hilo limeripuka likiwa ndani ya basi.(MM)
Mabaki ya
 maiti za watu zilizorowa damu ilikuwa imetapakaa kila mahala wakati 
vikosi vya usalama vikihangaika kudhibiti umma wa watu uliokuwa umezonga
 kutaka kujuwa kilichojiri na askari wa zima moto wakilimwagia maji basi
 ambalo bado lilikuwa na miili ya abria ilitoketea.
Rais Jonathan aapa kuwashinda Boko Haram
Shambulio
 hilo linaonyesha jinsi ilivyo rahisi kwa mji huo mkuu wa Nigeria kuweza
 kushambuliwa ambao umejengwa katika miaka ya 1980 kwa kuzingatia umbo 
la kijiografia ya nchi kuchukuwa nafasi ya mji wa Lagos kama makao makuu
 ya serikali katika nchi hiyo ambayo hivi sasa ndio yenye nguvu kubwa 
kabisa za kiuchumi barani Afrika na mzalishaji mkuu wa mafuta.
Rais 
Goodluck Jonathan wa Nigeria ameapa kwamba nchi hiyo itaushinda uasi huo
 wa kinyama wa kundi la Boko Haram wakati akitembelea eneo kulikotokea 
mripuko huo katika kituo cha basi.
Jonathan 
akizungumuza kwenye kituo hicho cha basi cha Nyanya kilioko kwenye 
viunga vya mji mkuu wa Abuja amesema wamepoteza watu kadhaa na kwamba 
suala hilo la Boko Haram ni historia mbaya kabisa inayotokea ndani ya 
kipindi cha maendeleo ya nchi hiyo lakini watawashinda Boko Haram na 
kwamba suala hilo ni la mpito.
Kuongezeka mashambulizi
Wanamgambo
 wa Boko Haram wanopigania kuanzishwa kwa taifa la Kiislamu wamejikita 
zaidi katika eneo la mbali la kaskazini mashariki ambapo wamekuwa 
wakiendesha harakati zao katika kipindi cha miezi kadhaa iliopita na 
wamekuwa wakizidi kuwalenga raia katika mashambulizi yao ambao 
wanawatuhumu kwa kutowa ushirikiano wao kwa serikali na vikosi vya 
usalama.
Meja 
Yahya Shinku afisa wa zamani katika jeshi la Nigeria anazungumzia kwa 
nini mashambulizi hayo yamekuwa yakizagaa kutoka nje ya eneo la 
kaskazini mashariki. Amesema "Baadhi ya mashambulio haya yamechochewa 
kisiasa na hayawezi kutenganishwa na ukweli kwamba tunaelekea kwenye 
uchaguzi wa mwaka 2015 ambapo kuna watu wana maslahi yao.
Baadhi ya
 watu wanaona shambulio hilo sio la kushangaza kwani hali ilikuwa 
ikizidi kuwa mbaya na huo ni kama ujumbe kwamba kundi hilo la Boko Haram
 bado lingalipo na linaweza kushambulia Abuja wakati wanapotaka na 
kusababisha hofu.
Mwandishi : Mohamed Dahman/Reuters/AFP
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman
CHANZO:DW
No comments:
Post a Comment