TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, October 22, 2014

Unamfahamu mmiliki wa kituo cha redio aliyefungwa? Picha na habari viko hapa

Malik
Mahakama ya Somalia imetoa amri ya kuzuiwa kwa pasipoti ya mmiliki wa kituo maarufu cha redio nchini humo, ambaye anakabiliwa na shtaka la kuhatarisha usalama wa nchi hiyo.
BBC inaripoti kuwa Abdimalik Yusuph mmiliki wa kituo cha redio Shabelle, ambaye ni raia wa Uingereza aliachiliwa kwa dhamana na kuamriwa kukabidhi pasipoti yake mahakamani kama dhamana, huku mwandishi mwingine akiendelea kushikiliwa na jeshi la polisi.
Abdimalik Yusuph, mmiliki wa kituo cha redio kilichofungiwa Somalia.
Abdimalik Yusuph, mmiliki wa kituo cha redio kilichofungiwa Somalia.
Waandishi hao ni miongoni mwa waandishi wa habari 4 wanaoshikiliwa na jeshi la polisi nchini Somalia wakikabiliwa na shitaka hilo baada ya kuripoti kuhusu mkakati wa Serikali ya nchi hiyo wa kuwapokonya silaha watu mjini Mogadishu.
Nchi ya Somalia inatajwa kuwa ni moja ya nchi yenye mazingira hatari zaidi kwa waandishi wa habari.
Waandishi wa habari wamelaani kitendo cha wenzao kushikiliwa na jeshi la polisi kwa zaidi ya miezi 3 bila ya kufunguliwa mashtaka, kinyume na katiba ya nchi hiyo.
Mahakama nchini humo imeahirisha kusikilizwa kwa kesi hiyo mpaka baada ya wiki mbili.

No comments:

Post a Comment