Taarifa nyingine kuhusiana kesi ya kuanguka kwa kanisa la T.B Joshua

Serikali ya jimbo la Lagos Nigeria, imesema sehemu ya jengo lililoaanguka katika kanisa la Synagogue Church of All Nations, ambalo lilijengwa kwa ajili ya kufikia wageni lilijengwa bila kibali cha Serikali.
Kamishna anayesimamia mipango miji 
Lagos, Olutoyin Ayinde amesema uchunguzi uliofanywa na tume iliyoongozwa
 na Oyetade Komolafe umeonyesha hakuna kibali kilichotolewa na mamlaka 
hiyo kuidhinisha ujenzi wa jengo la ghorofa sita.
Amesema kibali kilichotolewa kilikuwa 
cha ujenzi wa jengo la kanisa ambalo ni ukubwa wa ghorofa tano pekee, na
 uchunguzi umebaini kibali hicho kilikiukwa kwa kujengwa ghorofa nane 
badala ya tano.
Anyinde amesema mamlaka hiyo imeagiza 
mamlaka ya anga kuchunguza juu ya ndege ambayo imedaiwa kuzunguka jengo 
hilo muda mfupi kabla ya jengo kuanguka.
Kesi
 hiyo inayosikilizwa mahakama kuu Lagos imeahirishwa mpaka Novemba 5 
ambapo T.B Joshua atatoa ushahidi. Jengo hilo lilianguka Septemba 12 na 
kuua watu 116.

No comments:
Post a Comment