TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, October 31, 2014

Taarifa nyingine kuhusiana kesi ya kuanguka kwa kanisa la T.B Joshua

Synagogue-Collapse-BellaNaija1
Serikali ya jimbo la Lagos Nigeria, imesema sehemu ya jengo lililoaanguka katika kanisa la Synagogue Church of All Nations, ambalo lilijengwa kwa ajili ya kufikia wageni lilijengwa bila kibali cha Serikali.
Kamishna anayesimamia mipango miji Lagos, Olutoyin Ayinde amesema uchunguzi uliofanywa na tume iliyoongozwa na Oyetade Komolafe umeonyesha hakuna kibali kilichotolewa na mamlaka hiyo kuidhinisha ujenzi wa jengo la ghorofa sita.
Amesema kibali kilichotolewa kilikuwa cha ujenzi wa jengo la kanisa ambalo ni ukubwa wa ghorofa tano pekee, na uchunguzi umebaini kibali hicho kilikiukwa kwa kujengwa ghorofa nane badala ya tano.
Anyinde amesema mamlaka hiyo imeagiza mamlaka ya anga kuchunguza juu ya ndege ambayo imedaiwa kuzunguka jengo hilo muda mfupi kabla ya jengo kuanguka.
tb-joshua 
Kesi hiyo inayosikilizwa mahakama kuu Lagos imeahirishwa mpaka Novemba 5 ambapo T.B Joshua atatoa ushahidi. Jengo hilo lilianguka Septemba 12 na kuua watu 116.

No comments:

Post a Comment