TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, October 23, 2014

Canada yatoa tamko kuhusiana na shambulio la Bungeni.

Shambulio 
Masaa machache baada ya kutokea tukio la shambulizi la risasi katika bunge la Canada lililopelekea mwanajeshi mmoja na askari wa bunge, kuuawa serikali ya Canada imetoa tamko rasmi kuhusiana na tukio hilo.
Waziri mkuu wa Canada, Stephern Harper.
Waziri mkuu wa Canada, Stephern Harper.
Akitoa tamko hilo waziri mkuu wa Canada Stephen Harper amesema shambulio hilo ‘haliitetemeshi’ Canada, bali linaiongezea nchi hiyo ujasiri.
Rais wa Marekani Barack Obama na waziri mkuu wa Uingereza David Cameron wamelaani kitendo hicho kwa kukiita ni cha kukiita ni cha ‘kikatili’, huku wakisisitiza kuwa wakati huu ni wa kuwa macho zaidi kwa kuimarisha ushirikiano baina yao katika kupambana na ugaidi.
Cameron ameeleza kuwa tayari kushirikiana na Canada kwa msaada wowote utakaohitajika katika kukabiliana na hali hiyo.
Taarifa kutoka shirika la utangazaji nchini Ufaransa RFI linasema bado askari polisi wa kikosi maalum cha usalama wameendelea kulizunguka eneo hilo japo hali ya usalama imeimarika kwa sasa.
Canada imesema waliouawa kutokana na shambulio hilo ambao ni mwanajeshi koplo Nathan Cirillo na aliyekuwa askari wa bunge Kevin Vickers wamekufa kishujaa, huku polisi wakiendelea kumsaka mshukiwa wa tukio hilo aliyetajwa kwa jina la Michael Zehalf- Bibeau.
Kevin Vicker, askari wa bunge aliyeuawa kwa kupigwa risasi katika shambulio hilo
Kevin Vicker, askari wa bunge aliyeuawa kwa kupigwa risasi katika shambulio hilo
Koplo Nathan Cirillo , mwanajeshi aliyeuawa kwa kufyatuliwa risasi akiwa analinda katika makumbusho ya vita ya dunia jirani na jengo la Bunge la Canada.
Koplo Nathan Cirillo , mwanajeshi aliyeuawa kwa kufyatuliwa risasi akiwa analinda katika makumbusho ya vita ya dunia jirani na jengo la Bunge la Canada.

No comments:

Post a Comment