TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, October 6, 2014

MBUNGE MGIMWA ;VYOMBO VYA HABARI ELIMISHENI JAMII JUU YA KATIBA MPYA 


Mwenyekiti wa kamati ya  harambee ya  kuichangia  radio Maria  mkoa  wa Iringa Paschal Bella  kushoto akimpongeza  mbunge wa  jimbo la kalenga  Godfrey Mgimwa kwa  kuichangia radio maria  Tsh  milioni 1.5  leo  alipokuwa mgeni rasmi katika harambee  hiyo 

Mbunge  Mgimwa  akipongezwa  baada ya  kuchangia milioni 1.5 radio Maria  leo 

Mbunge wa Kalenga Bw Mgimwa akikabidhi lapto kwa mlezi wa kwaya Msindo mzee Mtandi (P.T)

Mtandi  akifurahi na mbunge wake Mgimwa 


Furaha ya  kukabidhiwa lapto

Mbunge wa  jimbo la kalenga Godfrey Mgimwa akivishwa kitenge cha Radio maria na mwenyekiti wa kamati ya kuchangia radio Maria Iringa  Paschal Bella  kushoto na katibu wake Martin Simangwa  leo 

Mgimwa akipongezwa  


VYOMBO  vya  habari  zatakiwa  kuepuka  kupotosha  umma  juu ya mchakato  mzima  wa  bunge la katiba  lililomalizika jana mjini  Dodoma.
Kauli  hiyo  imetolewa  leo katika  viwanja  vya kanisa la Rc Mshindo na mbunge wa  jimbo la kalenga  Godfrey  Mgimwa  wakati akichangia  kiasi cha Tsh  milioni 1.5  wakati wa harambee ya  kuichangia radio  Maria .
Alisema  kuwa iwapo  vyombo  vya  habari  zitatumika  vibaya  kuna  uwezekano  wa Taifa  kuingia  katika machafuko kama  zilizo nje  nyingine  na kama  vyombo  vya habari vitafanya kazi yake kwa  kuzingatia misingi ya maadili jamii itaunganishwa na vyombo  hivyo.
“ Radio  Maria  ni moja kati ya radio ambazo nimekuwa  nikizifuatilia  toka nikiwa  mdogo  na  nimekuwa  nikipenda  zaidi  jinsi  radio hiyo inavyofanya  shughuli  zake  na mbali ya  kufanya kazi ya  kueneza injili bado  imekuwa msaada  mkubwa  katika  kuelimisha umma……. Hivyo  rai yangu kwa radio  maria  ni kuona  inaendelea   hivyo  hivyo na ikiwezekana  kuandaa vipindi kwa ajili ya elimu kwa umma juu ya katiba  mpya “
Alisema  kuwa  wajumbe wa bunge la katiba  wametimiza kazi  yao ambayo  umma ulitegemea  kutoka  kwa  wajumbe hao  hivyo kazi   iliyobaki ni ya  wananchi  kucha  kuipitisha katiba   hiyo mwaka 2016 na  kuwa kwa wakati huu ni  vema vyombo  vya habari  kuendelea  kutoa  elimu kwa  umma juu ya kazi nzuri  iliyofanywa na  bunge  hilo la katiba .
Hata  hivyo  alisema ni  vema  watanzania  kuepukana na  watu  wachache  wasiolitakia mema Taifa  ambao  wanataka  kuona  nchi haitawaliki kwa  kutaka maandamano yasio  na tija  kwa jamii.
Mgimwa  alisema kuwa  njia pekee ya  kuepukana na  viongozi   wasio litakia  mema  taifa ni  pale  ambapo  vyombo  vya habari vitakapoweka msimamo wa uzalendo kwa  kuepuka  kuwa  sehemu ya kuhamasisha kuvunjika kwa amani  nchini.
Kwa  upande wake  mwenyekiti  wa kamati ya maandalizi ya harambee  hiyo Bw  Pascal Bella akishukuru  kwa  mchango  huo wa mbunge  Mgimwa  alisema  kuwa  mbali ya  kuwa  mbunge  huyo ni  wa jimbo la kalenga  ila  amekuwa msaada  mkubwa kwa kufanikisha zoezi  hilo la kuichangia radio hiyo.
Bella  alisema  kuwa  kila  mwaka  na kila  wakati  wadau  wa Radio  maria  wamekuwa na utaratibu  wa  kuichangia  radio  hiyo ambayo  uendeshaji  wake  unategemea  michango  kutoka kwa  wadau mbali mbali na  kuwa kwa  mwaka huu mkoa  wa Iringa pekee  unataraji  kuchangia  zaidi ya Tsh milioni 30

No comments:

Post a Comment