TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, October 22, 2014

T.I kufika Marekani si akakutana na mwandishi aliemuuliza kuhusu Ebola Tanzania… alichojibu kiko hapa

Screen Shot 2014-10-22 at 9.29.15 AM
Alikua mgeni kwenye stage ya Tamasha la Fiesta lililofanyika Leaders club October 18 2014 akiwa na timu yake ya watu wasiopungua watano na kuisimamia hiyo show kwa zaidi ya dakika 60.
Baada ya show Jumamosi, T.I aliondoka Tanzania Jumapili kurudi kwao Marekani kwa ajili ya kuhakikisha promo inakwenda vizuri sababu album yake mpya ilikua inatoka Jumanne ya October 21.
Akiwa NewYork T.I alijikuta yuko mbele ya camera akihojiwa na mwandishi wa habari aliemuuliza kuhusu ishu ya Iggy na Snoop ambayo alisaidia kuimaliza na baada ya hapo akamuuliza T.I vp Tanzania ilikuaje? Ebola je?
T.I alichojibu ni hiki >>>Tanzania ilikua poa sana, sijaona Ebola yoyote wala kuona hata dalili za kuwepo kwa ugonjwa huo, sijaona chochote cha kunifanya niifikirie Ebola au kuhisi uwepo wake

Muda mfupi kabla ya T.I kuja Tanzania ziliripotiwa stori kwamba rapper huyu amekua kiburi kwa kuamua kwenda Afrika pamoja na kwamba bara hili limekumbwa na ugonjwa hatari wa Ebola.
Mtandao wa TMZ uliripoti kwamba Management ya T.I imesisitiza ni lazima mkali huyu afanye hiyo show ya Fiesta na kwamba hakuna dalili zozote za Ebola kwenye ardhi ya Tanzania.
TMZ walizidi kuripoti kwamba Utafiti wa Oxford University ulisema Tanzania ni miongoni mwa nchi 15 za Afrika zilizo kwenye hatari ya kukumbwa na Ebola na ndio maana walishauri kama ingekua noma basi T.I afanye show akiwa kwenye puto kama Akon.
Screen Shot 2014-10-22 at 10.40.58 AM
Screen Shot 2014-10-22 at 12.11.05 PM

No comments:

Post a Comment