FC Barcelona yaweka rekodi ya kucheza mechi 7 bila kufungwa goli
FC 
Barcelona jana usiku ilicheza mechi yake ya 7 katika ligi kuu ya 
Hispania bila kupoteza mchezo wowote, wakishinda mechi 6 na kutoa sare 
moja.
Lionel 
Messi alifunga goli lake 402 tangu aanze kucheza soka la ushindani na 
baadae akamtengenezea Neymar aliyehitimisha ushindi wa 2-0 dhidi ya Rayo
 Vallecano.(P.T)
Kutokana 
na ushindi huo kikosi cha Luis Enrique sasa kimefanikiwa kuwa timu ya 
kwanza katika historia ya La liga kucheza mechi 7 za mwanzoni mwa ligi 
hiyo bila kuruhusu wavu wao kugushwa.
Pia wakati huo huo golikipa wa timu hiyo, Mchile Claudio Bravo ameweka rekodi mpya ya katika kulinda lango lake.
Bravo 
amevunja rekodi ya kucheza dakika nyingi bila kuruhusu wavu wake 
kuguswa, mpaka kufikia sasa Bravo amecheza jumla ya dakika 561 bila 
kufungwa goli, akivunja rekodi ya golikipa wa zamani wa Barca, Pedro 
Artola aliyecheza kwa dakika 560 bila kufungwa goli katika msimu wa  
1977-78.

No comments:
Post a Comment