Msichana asimulia ya Boko Haram

Baadhi ya wasichana waliotekwa nyara
Ni miezi 
sita sasa baada ya wanamgambo wa kiislam wa kundi la Boko Haram kuwateka
 wanafunzi wasichana Zaidi ya 200 kaskazini mashariki mwa Nigeria, 
wasichana watatu ambao wametoroka wamezungumza katika mahojiano maalum 
na idhaa ya Kihausa ya BBC.
Tukio 
hili linakuja wakati serikali ya Nigeria ikiwa katika makubaliano ya 
kusimamisha mapigano dhidi ya Boko Haram hatua itakayo saidia 
kuwaachilia huru wasichana waliotekwa na kundi hilo .
'' 
nilikuwa nataka kurukia nje wakati msichana mwenzangu aliponikamata kwa 
nyuma na kusema watakupiga risasi kama utafanya hivyo. Nikasema, nini 
utofauti wataniua mimi hapa na kuacha maiti yangu ikusachukuliwa 
nilikuwa nalia na kuomba mpaka tulipoifikia kambini" Anasimulia msichana
 mmoja alitoroka mikononi mwa Boko Haram.(P.T)
Akizungumza
 katika mahojiano maalum na idhaa ya Kihausa ya BBC, Msichana huyu 
anakumbuka jinsi alivyokuwa nyuma ya Lori wakati wanapinaji wa Boko 
Haramu walipomteka yeye na wasichana wengine.
Zaidi ya 
wasichana 200 kati miongoni mwao walikuwa walitekwa lakini wale 
waliokimbia walibahatika kutoingia katika hofu kubwa kwenye mikono ya 
watekaji.
Shirika 
la kimataifa la kutetea haki za binaadam la Human Rights Watch limesema 
wanawake wanaoshikiliwa na kundi la Boko Haramu wamekuwa wakinyanyaswa, 
kubakwa na hata kulazimishwa kuolewa.
Katika 
ripoti mpya ya shirika hilo inasema Wanamgambo hao wa Kiislam 
wamewawateka wanawake Zaidi ya 500 na wasichana tangu mwaka 2009.
Serikali 
ya Nigeria hivi karibuni imetangaza makubaliano ya kusimamisha mapigano 
dhidi ya Boko Haram ambayo hatua itakayawafanya wanamgambo ho kuachilia 
huru wasichana wa hao waliotekwa huko Chibok.
Lakini 
Boko Haram wenyewe hawajawahi kuthibitisha makubaliano yoyote ya 
kusitisha mapigano na hakuna dalili zozote za kuachiwa kwa wasichana 
haohivi karibuni.
Lakini kwa wale waliobahatika kutoroka, matatizo ya kisaikolojia bado yanawasumbua..
No comments:
Post a Comment