Mgonjwa wa Ebola agundulika Newyork

Mji wa Newyork
Daktari 
wa Marekani aliyekuwa akiwahudumia wagonjwa wa Ebola Nchini Guinea 
amepimwa na kukutwa na virusi vya ugonjwa huko katika hospitali ya ya 
mjini Newyork.
Dr Craig 
Spencer ambaye ni mmoja kati ya madaktari wasio na mipaka alianza 
kujisikia maumivu na homa siku chache tu baada ya kurejea Marekani 
akitokea Afrika Magharibi.BBC
Siku ya Alhamisi wiki hii Craig alipelekwa hospitali kwaajili ya vipimo na kisha akatengwa kwa uchunguzi zaidi wa afya yake.
Katika 
taarifa yake kwa vyombo vya habari Meya wa mji wa Newyork Bill de Blasio
 amesema watu hawapaswi kuwa na hofu kwani hatua zote mhimu zilifuatwa 
katika kumchunguza Dr.Craig na hadi alipobainika kuwa na maambukizi 
hayo.
Kubainika
 kuwa na virusi vya ugonjwa wa Ebola kwa Dr.Craig kunaongeza idadi ya 
waliobainika kuwa na ugonjwa huo nchini Marekani kutoka watatu na 
kufikia wagonjwa wanne.
No comments:
Post a Comment