SHIRIKISHO LA MUZIKI TANZANIA LATOA PONGEZI KWA BUNGE MAALUM LA KATIBA
Na Anitha Jonas –Maelezo.
SHIRIKISHO
 la Muziki Tanzania limetoa pongezi za dhati kwa Bunge Maalum la Katiba 
lililokuwa likiongozwa na Mwenyekiti wa Bunge hilo Mhe. Samuel Sitta kwa
 kuingiza Ibara tatu katika Rasimu ya Katiba inayopendekezwa huko mjini 
Dodoma.
Pongezi 
hizo zilitolewa jana na Rais wa Shirikisho hilo Bw. Addo November 
alipokuwa akiongea na Waandishi wa habari hapo jana huku akisema kuwa 
Rasimu Inayopendekezwa imezingatia haki za Wasanii kwa kuingiza Ibara 
tatu zikiwemo Ibara ya 15, ya 38 (II) na Ibara ya 56, 3 (e) ambazo Ibara
 hizo zinalinda kazi za muziki na sanaa zote kwa ujumla.(Martha Magessa)
Bw. 
November alieleza kuwa Shirikisho limefurahi kuona kuwa Sheria ya 
inayohusu masuala ya kazi za sanaa katika nchini imeanza kutekelezwa 
Kikatiba kama ilivyo katika nchi mbalimbali zikiwemo Marekani, Rwanda na
 Uingereza.
"Kwa 
kubainisha ibara hizi katika Rasimu ya Katiba Inayopendekezwa, 
zinaonyesha ulindaji wa Hati Miliki (Intellectual property) za Wasanii 
na kazi zao na hii itasaidia kuboresha maisha ya wasanii kimapato kwa 
kupitia kazi zao kwani Katiba hii itawalinda wasanii Kisheria", alisema 
November.
Aliongeza
 kuwa Shirikisho limeingia Mkataba na Kampuni ya JB Belmont kwa kuweza 
kuwapatia wasanii na waandishi wa habari punguzo la bei katika huduma 
mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo.
Aidha, 
November aliwashauri waandishi wa habari kuunda Shirikisho la Waandishi 
wa habari la muziki kwani hii itasaidia kupata na kutoa taarifa 
mbalimbali kwa jamii zinazohusu masuala ya muziki kwa kuaangalia 
walikotoka na wanakoelekea kimaendeleo.
Naye 
Meneja Mahusiano wa Kampuni ya JB Belmont, Bi. Gillian Macheche alisema 
kuwa kutakuwa na punguzo la asilimia 40 kwa huduma mbalimbali ikiwemo 
kukodi Ukumbi wa Mkutano, Vyumba vya kulala wageni, vyakula na Vinywaji 
kwa wasanii na waandishi wa habari.
Kwa 
upande mwingine Mjumbe wa Shirikisho hilo ambaye pia ni Mwanamuziki 
mkongwe nchini Bw. Kassim Mapili alitoa shukrani zake za dhati kwa 
waandishi wa habari kwa kutoa taarifa kwa umma juu ya afya yake pamoja 
na jamii kwa ujumla kwa kumsaidia katika kipindi chote alichokuwa 
akitibiwa ugonjwa wa Moyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili
No comments:
Post a Comment