Hii ndiyo taarifa iliyotolewa na FIFA kuhusiana na Ebola
Shirikisho
 la soka Duniani FIFA limesema mashindano ya kombe la dunia la FIFA kwa 
ngazi ya vilabu yanayotarajiwa kufanyika mwezi Desemba mwaka huu 
yataendelea kama ilivyopanga, huku likisisitiza vilabu vyote kuhusiana 
na kuchukua tahadhari juu ya virusi vya Ebola pindi inapofanyika 
michuano hiyo ya kimataifa.
Kitendo cha baadhi ya nchi kukumbwa na 
janga la Ebola kuliibua maswali namna ambavyo michuano hiyo itawezekana 
kufanyika na pia juu ya usalama wa wachezaji hasa pale ambapo 
watalazimika kwenda kucheza mechi katika moja ya nchi ambayo iko kwenye 
ukanda ulioathirika na ugonjwa huo.
FIFA imewatoa wasi wasi kwa kutoa ushauri namna ambayo itasaidia kupunguza hatari ya kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa huo.
Mbali ya mapendekezo yaliyotolewa na 
FIFA ya kufanya vipimo vya afya za wachezaji wa vilabu husika baada ya 
kurejea kutoka moja ya nchi ambayo iko katika ukanda ulioathiriwa na 
Ebola, na kushauri naadhi ya mechi ambao zilipangwa kufanyika Guinea, 
Sierra Leone na Liberia kuhamishiwa katika viwanja ambavyo vipo katika 
nchi zenye viwanja vyenye nafasi.
Mbali na FIFA kusisitiza kuwatenga 
haraka wachezaji watakaoonesha dalili za Ebola wakati ikifanyika 
michuano ya kimataifa, vile vile imewataka wachezaji kutoka nchi 
zilizoathirika kuwa na tahadhali kubwa kwa kupima afya zao.

No comments:
Post a Comment