TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, October 29, 2014

Hii ndiyo taarifa iliyotolewa na FIFA kuhusiana na Ebola

Fifa-headquarters-007 
Shirikisho la soka Duniani FIFA limesema mashindano ya kombe la dunia la FIFA kwa ngazi ya vilabu yanayotarajiwa kufanyika mwezi Desemba mwaka huu yataendelea kama ilivyopanga, huku likisisitiza vilabu vyote kuhusiana na kuchukua tahadhari juu ya virusi vya Ebola pindi inapofanyika michuano hiyo ya kimataifa.
Kitendo cha baadhi ya nchi kukumbwa na janga la Ebola kuliibua maswali namna ambavyo michuano hiyo itawezekana kufanyika na pia juu ya usalama wa wachezaji hasa pale ambapo watalazimika kwenda kucheza mechi katika moja ya nchi ambayo iko kwenye ukanda ulioathirika na ugonjwa huo.
FIFA imewatoa wasi wasi kwa kutoa ushauri namna ambayo itasaidia kupunguza hatari ya kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa huo.
Mbali ya mapendekezo yaliyotolewa na FIFA ya kufanya vipimo vya afya za wachezaji wa vilabu husika baada ya kurejea kutoka moja ya nchi ambayo iko katika ukanda ulioathiriwa na Ebola, na kushauri naadhi ya mechi ambao zilipangwa kufanyika Guinea, Sierra Leone na Liberia kuhamishiwa katika viwanja ambavyo vipo katika nchi zenye viwanja vyenye nafasi.
Mbali na FIFA kusisitiza kuwatenga haraka wachezaji watakaoonesha dalili za Ebola wakati ikifanyika michuano ya kimataifa, vile vile imewataka wachezaji kutoka nchi zilizoathirika kuwa na tahadhali kubwa kwa kupima afya zao.

No comments:

Post a Comment