T.I amehojiwa tena Marekani na kuzungumzia mengine mapya kuhusu Tanzania 
Clifford
 Joseph Harris, Jr. a.k.a T.I mkali kutoka Marekani aliyeangusha show ya
 nguvu katika jukwaa la Fiesta 2014 siku ya Jumamosi Oktoba 18 2014 
katika viwanja vya Leaders Club Dar es Salaam, bado ameendelea 
kuyasimulia mazuri na makubwa ya kuvutia aliyokutana nayo Tanzania.
Katika mahojiano aliyofanya New York Marekani na kituo maarufu cha redio Power 105.1
 kwenye show ya Breakfast Club, T.I amesema tangu aanze kufanya muziki 
hajawahi kufanya show kwenye jukwaa lolote mbele ya mashabiki zaidi ya 
50,000.
T.I amelinganisha idadi hiyo kubwa 
aliyokutana nayo Tanzania kuwa ni sawa na kufanya show katika uwanja wa 
mpira wa miguu na kuujaza kwa show moja, kitu ambacho anakiona kabisa 
sio rahisi na ndio maana hii ya Leaders imekua kubwa kwake.
Swali la kuhusu Ebola bado liliulizwa 
kwa T.I kama alichukua tahadhari kwa kufanya utafiti kabla ya kwenda 
Afrika na kusema hakuwa na hofu yoyote alipokuja Tanzania, zaidi alikuwa
 akifikiria tu kuhusu mpenzi wake, hata hivyo hakukutana na Ebola wala 
kuona hata dalili za uwepo wake na kusisitiza kwamba mara nyingi Ebola 
imekua ikiwapata Wanaowahudumia wagonjwa’
Kwenye sentensi nyingine rapper huyu 
mwenye umri wa miaka 34 alisifia jinsi alivyopokelewa vizuri na kusema 
Tanzania ni watu wazuri hivyo akamwambia Dj Envy kwamba ataenjoy sana 
kwenye safari yake ya Afrika December mwaka huu.

No comments:
Post a Comment