TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Saturday, September 28, 2013

WAKAGUZI WA UN WA SILAHA ZA KEMIKALI WAREJEA SYRIA

sumu 644f4
Wakaguzi wa silaha za kemikali wa Umoja wa Mataifa wamerejea Syria kufanya uchunguzi wa matumizi ya silaha hizo zilizopigwa marufuku nchini humo wakati wa miaka miwili na nusu ya vita vya wenyewe kwa wenyewe. (HM)

Kundi linaloongozwa na Ake Sellstorm lilikwenda nchi jirani ya Lebanon jumatano na kusafiri kwa kutumia gari hadi Damascus.
Kwanza walikwenda Syria mwezi uliopita kufanya uchunguzi wa mashambulizi matatu ikiwemo lile la mwezi Machi nje ya mji wa Aleppo ambalo serikali ya Syria na wapiganaji waasi wanashutumiana.
Kundi hilo lilihamisha mwelekeo wake wa ujumbe wa wiki mbili na kuzingatia shambulizi jipya nje ya Damascus ambako waligundua kwamba silaha za kemikali zilitumika.
Wakati huohuo Jumatano kundi la waasi 13 lilitoa taarifa ya pamoja kupinga baraza la upinzani la taifa la Syria likisema kuwa haliwakilishi tena ushawishi wao.
Watu wengi waliokimbia nchi hiyo wamekwenda nchi jirani ikiwemo Jordan, Lebanon, Uturuki na Iraq. Chanzo: bbcswahili

No comments:

Post a Comment