TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, September 30, 2013

SUAREZ AFUNGA 2 LIVERPOOL IKIIUA SUNDERLAND 3-1 

suarez debd5
Luis Suarez akishangilia kwa kuonyesha picha ya mkewe na binti yake na mtoto wake mpya wa kiume, Benjamin (HM)

suarez2 9aaee
MSHAMBULIAJI Luis Suarez amerejea na moto katika Ligi Kuu ya England baada ya kumaliza adhabu yake ya mechi 10, leo akifunga mabao mawili katika ushindi wa 3-1 wa Liverpool dhidi ya Sunderland.
Ntyota huyo wa Uruguay alifunga mabao yake katika dakika za 36 na 89 wakati lingine lilifungwa na mshambuliaji pacha wake, Daniel Sturridge dakika ya 28 na kufutia machozi la wenyeji lifungwa na Emanuele Giaccherini dakika ya 52.
Kikosi cha Liverpool kilikuwa: Mignolet, Toure, Skrtel, Sakho, Henderson, Gerrard, Lucas, Jose Enrique, Moses/Sterling dk75, Sturridge na Suarez.
Sunderland: Westwood, Gardner, O'Shea, Cuellar, Colback, Larsson/Mavrias dk85, Cattermole/Celustka dk74, Ki,Johnson, Altidore na Giaccherini.

No comments:

Post a Comment