TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, September 24, 2013

Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi yaelezea kuhusu mikakati ya Serikali; 

 a1_ade17.png

Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini wakitazama moja ya mabwawa yanayotumika kufugia samaki katika mradi unaoendeshwa na William Bwemelo katika eneo la Pugu Kinyamwezi kwa msaada wa Wataalamu wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi.
a2_c082a.png
Msemaji wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Mohamed Bahari akiwaeleza waandishi wa habari kuhusu mikakati ya Serikali katika kukabiliana na upungufu wa samaki nchini kwa kutoa msukumo kwa wananchi kuanzisha miradi ya ufugaji wa samaki katika maeneo yao. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi Bahari Kuu Zahor El Kharousy.(P.T)
a3_8bc85.png
Baadhi ya Waandishi wa habari wakisikiliza maelezo toka kwa Msemaji wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Mohamed Bahari akiwaeleza kuhusu mikakati ya Serikali katika kukabiliana na upungufu wa samaki nchini wakati walipotembelea moja ya miradi ya ufugaji samaki katika eneo la Pugu Kinyamwezi jijini Dar es Salaam.
a4_94655.png
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maendeleo ya Uvuvi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Fatma Sobo akiwaeleza waandishi wa habari juu hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kupambana na Uvuvi haramu hapa nchini.
a5_8c87d.png
Mtafiti Mwandamizi kutoka Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI) Dr. Baraka Kuguru akifafanua kwa waandishi wa habari namna bora ya kukuza vifaranga vya samaki wakati walipotembelea mradi huo.

No comments:

Post a Comment