MISS UTALII KUTANGAZA KUPATIKANA NYATI WA AJABU NGORONGORO

Nyati mweupe nayepatikana Ngorongoro (HM)

Miss Utalii Tanzania 2013, Hadija Said
 Mswaga, amesema kuwa kupatikana kwa nyati mweupe wa ajabu na pekee 
duniani katika hifadhi ya Ngorongoro, imekuwa ni chachu na kichocheo cha
 pekee kwake katika mpango mkakati wake wa kuitangaza Hifadhi ya 
Ngorongoro kitaifa na kimataifa, ambapo kwa kuanzia ameamua kuanza 
kampeni hiyo kupitia mashindano ya dunia anayokwenda kushiriki ya Miss 
Tourism World 2013, ambayo mwaka huu yanafanyikia nchini Equatorial 
Guinea Octoba 12, 2013.
Kupatikana kwa Nyati huyo wa ajabu 
Mweupe, ambaye hapatikani sehemu nyingine yoyote Duniani, wakati huu 
ambao anakwenda katika mashindano hayo ya Dunia, imekuwa ni fulsa ya 
pekee kwa Tanzania, Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na kwake , 
kuithibitishia dunia kuwa Ngorongoro Cater ni Ajabu la Asili la Dunia 
Barani Afrika. Ambapo sasa Ngorongoro Crater pamoja na maajabu ya bonde 
lenyewe la kreta ya Ngorongoro, pia kuna maajabu ya Nyati Mweupe, Unyayo
 wa Binadamu wa kale zaidi Duniani, Mchanga wa ajabu unao hama kila 
mwaka kwa umbo la Nusu mwezi, Mlima wenye Volkano Hai wa Oldonyo Lengai,
 lakini pia ushirikiano wa kuishi bila kudhuriana wa binadamu na Wanyama
 katika hifadhi hiyo na upatikanaji wa jamii karibu zote za Wanyama 
wakubwa (BIG FIVE) na adimu duniani wakiwemo Faru Weusi,Duma,Mbwa Mwitu,
 Kaka kuona n.k.
Ngorongoro Crater na Hifadhi nzima ya 
Ngorongoro ni tunu ya Taifa la Tanzania, nahazina ya Dunia ambayo 
tunapaswa kuienzi na kuitangaza kwa nguvu zetu zote, ili iweze kuingiza 
pato na kuchangia zaidi uchumi na pato la Taifa, lakini pia kukuza na 
kuendeleza huduma za jamii ,ikiwemo elimu na afya. Naupongeza uongozi wa
 Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) kwa jitihada zao za kukuza 
utalii na kupambana na majangili , nawaomba kuimarisha na kuongeza 
mapambano na vita dhidi ya ujangili na majangili, ili kuhakikisha kuwa 
majangili hao hawamdhuru nyati huyo wa ajabu na Wanyama wengine katika 
hifadhi hiyo. Lakini pia naiomba mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro 
kumlinda nyati huyo dhidi ya Wanyama wengine wala nyama kama samba n.k.
Wafanyakazi wa hifadhi hiyo Ijumaa ya 
tarehe 27-9-2013 asubuhi wakiwa katika basi la mamlaka wakienda kazini 
walimshudia Nyati huyo akiwa na kundi la nyati wengine kandokando ya 
barabara ndani ya hifadhi hiyo. Jambo ambalo liliwavutia na dereva wa 
basi hilo kulazimika kusimamisha basi kutoa fulsa kwa wafanyakazi hao 
kumshudia nyati huyo na baadhi yao kupiga picha kwa simu zao na kamera 
walizokuwa nazo.
Hadija ameushukuru uongozi wa 
Ngorongoro , kwa kumpatia DVD zaidi ya 100 ya hifadhi hiyo,ambazo 
atakwenda kuzigawa kwa washiriki wote 126 na vituo vya Televisheni vya 
nchi zao wanaoshiriki katika mashindano hayo ya Dunia ya Miss Tourism 
World 2013 mwaka huu. Baada ya kurudi nitazunguka nchi nzima na dunia 
nzima kuitangaza Ngorongoro kwa kushirikiana na Uongozi wa Miss Tourism 
Tanzania Organisation na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. Chanzo: 
fullshangweblog
No comments:
Post a Comment