Dk SHEIN AMPONGEZA RAIS WA CHINA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa 
Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein amemtumia salamu za pongezi 
Rais wa China, Xi Jinping kwa kuadhimisha miaka 64 ya Uhuru wa nchi 
hiyo.
Katika salamu zake hizo, Rais wa 
Zanzibar amesema wananchi wa Zanzibar wanaungana na ndugu zao wa China 
katika kusherehekea miaka 64 ya uhuru wa nchi hiyo pamoja na urafiki na 
mshikamano uliodumu kwa muda mrefu baina ya mataifa hayo mawili.(P.T)
            
Dk Shein ameitumia fursa hiyo 
kuipongeza Serikali ya China kwa mafanikio makubwa iliyoyapata katika 
sekta zote za maendeleo chini ya uongozi wa Chama cha Kikomunisti.
Ameelezea matumaini yake kuwa ushirikiano baina ya Serikali ya China na Wananchi wa Zanzibar utaendelea kuimarika zaidi.
                    
Ameelezea matumaini yake kuwa ushirikiano baina ya Serikali ya China na Wananchi wa Zanzibar utaendelea kuimarika zaidi.
No comments:
Post a Comment