Jaji Mutungi aiumbua CCM

HATIMAYE 
Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi ameanza kuonyesha 
makali, baada ya kukipa onyo kali Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kukitaka 
kuacha mara moja kutumia viongozi wa kidiplomasia kwenye shughuli za 
kisiasa.
Hatua ya 
Jaji Mutungi, imekuja siku chache baada ya CCM kumtumia Balozi wa China,
 Dk. Lu Youping katika shughuli za kisiasa mkoani Shinyanga wiki 
iliyopita.(hd)
Taarifa 
iliyotolewa kwa vyombo vya habari mjini Dar es Salaam jana, ilisema 
suala la ushiriki wa raia wa kigeni ikijumuisha wanadiplomasia katika 
shughuli za kisiasa nchini, halikubaliki.
Alisema 
ofisi yake, inaunga mkono kwa dhati hatua iliyochukuliwa na Serikali 
kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kukemea 
jambo hilo.
"Tamko la
 Serikali limezingatia sheria na wajibu wa wanadiplomasia, wakati wa 
uwepo wao hapa nchini, mimi nikiwa mlezi wa vyama vya siasa, ninakemea 
kitendo cha CCM kumshirikisha Balozi wa China katika shughuli za 
kisiasa," alisema Jaji Mutungi.
Alisema 
katika tukio hilo, CCM kuruhusu raia wa kigeni kutumia jukwaa lake ni 
dhahiri limezua hali ya taharuki kwa wananchi, japo sheria ya vyama vya 
siasa kwa upande wake iko kimya katika suala hilo.
"Naviasa 
vyama vya siasa kwa ujumla wake, kuzingatia na kufuata sheria na 
taratibu stahiki katika utekelezaji wa shughuli zao za kisiasa.
"Napenda 
kuujulisha umma kwamba, ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kwa wakati 
huu ipo kwenye mchakato wa marekebisho ya sheria husika ya vyama vya 
siasa, ambayo imebainika kuwa na upungufu....lengo ni kukabiliana na 
changamoto zilizopo likiwemo suala hili," alisema Msajili, Jaji Mutungi 
katika taarifa yake aliongeza sasa hivi ofisi yake inaendelea kukusanya maoni ya wadau katika jitihada za kufanikisha marekebisho ya sheria hiyo.
Suala la 
CCM kumshirikisha Balozi wa China katika masuala ya kisiasa, lilizua 
mjadala mkubwa hali iliyosababisha CHADEMA kutoa tamko na kuandika barua
 ya malalamiko UN wakitaka aondolewe kwa kupoteza sifa za kuwa balozi, 
baada ya kuvunja mkataba wa Umoja wa Mataifa wa 1961 unaosimamia nchi na
 nchi.
CHADEMA 
waliandika barua nyingine kwenda Serikali ya China na Tanzania, wakitaka
 msimamo na hatua zitakazochukuliwa dhidi ya balozi huyo kuvunja mkataba
 huo ibara ya 41(1-3), kinachokataza balozi kujihusisha na siasa katika 
Taifa ambalo yuko.
Chadema 
imesema inalaani kitendo hicho na itachukua hatua kwenda Umoja wa 
Mataifa na pia kupata maelezo toka Serikali ya China kama imemtuma 
balozi huyo kujihusisha na mambo ya siasa za ndani za vyama au 
kuiwakilisha nchi.
Akijibu 
tuhuma hizo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema 
alichofanya balozi huyo ni kitendo cha kuungwa mkono, maana alikuwepo 
kwa nia ya kuangalia maeneo ya uwekezaji wa zao la Pamba katika Mkoa wa 
Shinyanga.
Alisema 
uwekezaji kutoka China, utasaidia kuondoa tatizo sugu la ajira, kupanda 
kwa bei ya zao la pamba ambacho kimekuwa kilio kikubwa cha wakulima 
pamoja na ujengwaji wa viwanda vya nguo na kuchuja mafuta.
Hivyo ni 
vema kumpongeza balozi huyo na kuunga juhudi za CCM za kuwatafuta 
wawekezaji wa nje, badala ya kusingizia uvunjaji wa Mkataba wa Vienna 
ili kupata umaarufu wa kisiasa:chanzo mtanzania
No comments:
Post a Comment