-Alikuwa mke wa Lindsay, mtuhumiwa wa ugaidi jijini London
-Alikuwa anatafutwa na polisi wa Kenya kabla ya tukio la juzi
-Al-Shabaab wamtaja kuwa mwanamke shujaa
-Alipanga kumtorosha mwenzake aitwaye Grant leo
Habari: Clarence Mulisa na Mitandao
MWANAMAMA Samantha Lewthwaite amehusishwa katika shambulio la kigaidi lililotokea jijini Nairobi, juzi Jumamosi kwenye jengo la biashara la Westgate.
Lewthwaite anadaiwa kuwa miongoni mwa
magaidi 10-15 waliohusika katika tukio hilo lililopoteza maisha ya watu
69 mpaka sasa wakati zaidi ya 175 wakijeruhiwa.

Samantha Lewthwaite (29), maarufu kama
'Mjane Mweupe' ni Mwingereza aliyekuwa mke wa Germaine Maurice Lindsay
maarufu kwa jina la Abdullah Shaheed Jamal, mmoja wa magaidi kati ya
wanne waliojitoa mhanga katika shambulio la Julai 7, 2005 jijini London
lijulikanalo kama (7/7) lililoua watu 56 pamoja na wao na kujeruhi
zaidi ya 700.
Bomu la Lindsay liliua watu 26 baada ya kulipua treni ipitayo chini ya ardhi jijini London.
Lewthwaite, ambaye alibadili dini enzi za ujana wake na kuitwa Sherafiyah anadaiwa kuwa na watoto watatu.
Lewthwaite, ambaye alibadili dini enzi za ujana wake na kuitwa Sherafiyah anadaiwa kuwa na watoto watatu.
Serikali ya Kenya imeeleza kuwa baadhi ya
majeruhi waliookolewa kutoka katika jengo la Westgate walidai kumuona
mwanamke mweupe (aliyefanana na Lewthwaite) akiwa miongoni mwa magaidi
walioteka jengo hilo.
Al- Shabaab kupitia katika akaunti yao ya
Twitter wamemtukuza Lewthwaite kwa kusema yupo katika viwango vyao na
ni mwanamke shujaa.
Inasadikiwa kuwa mwanamke huyo alikuwa
mmoja kati ya viongozi wa magaidi hao baada ya askari kudai kuwa
mwanamke mweupe aliyekuwa amevaa hijabu alikuwa akitoa amri kwa wenzake
katika lugha ya Kiarabu wakati wa shambulio hilo.
Desemba 2011, askari nchini Kenya walibaini
kemikali za kutengeneza milipuko sawa na zile zilizotumika katika
milipuko ya Julai 7, 2005 jijini London katika vyumba viwili vya
kupangisha. Lewthwaite alidaiwa kuwa ndiye aliyekuwa amepangisha vyumba
hivyo japo hakukamatwa.
Katika tukio hilo, Mwingereza, Jermaine
Grant, alikamatwa akiwa jijini Mombasa kwa kuhusika na kemikali hizo.
Baada ya kukamatwa, Grant aliwaeleza askari wa Kenya kuwa anafanya kazi
chini ya Lewthwaite. Alikamatwa pamoja na mtu mwingine aliyekuwa
anajaribu kutoroka nchini Kenya.

Aprili 2012, ilithibitishwa kuwa mtuhumiwa
katika tukio hilo alikuwa Lewthwaite mwenyewe ambaye anadaiwa kuvuka
mpaka wa Kenya na kuja Tanzania akiwa na watoto wake watatu Desemba 26,
2011.
Machi mwaka huu, Daily Telegraph liliripoti kuwa Lewthwaite na Fouad
Manswab walikuwa wanapanga kumtorosha Grant na mpango wao ulipangwa
kufanyika leo Septemba 23, 2013 jijini Mombasa."Tunajua Fouad anawasiliana na Samantha Lewthwaite na walipanga kumuokoa mwenzao," alisema Jacob Ondari, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) wa Kenya kipindi hicho.
Katika ripoti mbalimbali, Lewthwaite anatajwa kuwa mfadhili, muongozaji na mwalimu wa Al Qaeda na muandaaji wa Kundi la Jihad kwa wanawake barani Afrika.
No comments:
Post a Comment