TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, September 20, 2013

SWANSEA YAICHAPA VALENCIA 3-0 EUROPA LEAGUE

toten2 982a3
Swansea wakishangilia bao
WAKALI wa soka ya kitabuni England, Swansea wameanza vyema Europa League baada ya kuifumua mabao 3-0 nyumbani kwake Valencia iliyomaliza na wachezaji 10. (HM)
Wenyeji walilazimika kucheza 10 kwa takriban dakika 80, baada ya beki Adil Rami kutolewa nje kwa kadi nyekundu, kufuatia kumchezea rafu Wilfried Bony.
Mshambuliaji huyo ndiye aliyeifungia Swansea bao la kwanza dakika ya 14 usiku huu, hilo likiwa bao lake la tano katika mechi nanemsimu huu.
Mabao mengine yalifungwa na Michu dakika ya 58 na Jonathan de Guzman dakika ya 62.
Kikosi cha Valencia kilikuwa: Guaita, Barragan, Rami, Feghouli/Pabon dk59, Mathieu, Ever/Costa dk14, Javi Fuego, Guardado, Canales/Bernat dk66, Cartabia na Postiga.
Swansea: Vorm, Rangel/Davies dk56, Amat, Chico, Tiendalli, de Guzman, Canas, Pozuelo, Dyer/Lamah dk65, Michu/Shelvey dk77 na Bony.
Katika mchezo mwingine, mabao mawili ya Jermain Defoe yalichgia ushindi wa 3-0 kwa Tottenham dhidi ya Tromso, bao lingine akifunga Christian Eriksen.
toten 7d48c
Pamoja na ushindi huo, Mousa Dembele, Danny Rose and Younes Kaboul wote walitoewa nje baada ya kuumia.
Tottenham ilimaliza mechi na wachezaji 10 kutokana na Kaboul kutolewa nje baada ya kuumia, wakati kocha Andre Villas-Boas amemaliza idadi ya wachezaji wa kubadili.
Spurs: Lloris, Naughton, Kaboul, Dawson, Rose, Sandro, Dembele, Sigurdsson, Holtby, Lamela na Defoe.
Tromso: Sahlman, Kristiansen, Fojut, Koppinen, Causevic, Bendiksen, Johansen, Drage, Pritchard, Moldskred, Ondrasek. Chanzo: binzubeiry

No comments:

Post a Comment