TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, September 30, 2013

MANCINI ATUA UTURUKI KUSAINI MKATABA WA KUINOA GALATASARAY 

 mancin2 49684

Roberto Mancini amekwenda Uturuki kwa ajili ya kusaini kuifundisha Galatasaray (HM)
mancin ce341
KOCHA Roberto Mancini jana amekwenda mjini Istanbul, Uturukikufanya mazungumzo ya kusaini Mkataba wa miaka mitatu kuifundisha Galatasaray utakaokuwa na thamani ya Pauni Milioni 4.6 kwa mwaka.
Mancini, amekuwa 'juu ya mawe' tangu atupiwe virago Manchester City mwishoni mwa msimu na anatarajiwa kutambulishwa kurithi mikoba ya Fatih Terim Jumanne.
Mabingwa hao wa Uturuki pia wamekubali kumlipa Mtaliano huyo bonasi ya Pauni Milioni 5.86 kama watavuka hatua waliyofika mwaka jana Ligi ya Mabingwa na kufanikiwa kuingia Robo Fainali.
Mancini anatarajiwa kukutana na Rais wa klabu, Unal Aysal Jumatatu kufikia makubaliano ya mwisho ya Mkataba, kwa mujibu wa wakala Muzzi Ozcan ambaye alifanikisha kuziunganisha pande hizo mbili, baada ya klabu hiyo kumfukuza Terim. Chanzo: binzubeiry

No comments:

Post a Comment