RAIS OBAMA ANAELEKEA AFRIKA KUSINI

RAIS wa Marekani Barack Obama leo 
Ijumaa anaelekea Afrika Kusini ambapo miongoni mwa shughuli zake atazuru
 kisiwa cha Robben Island  alikozuiliwa jela rais wa zamani Nelson 
Mandela kwa miaka 27.
Rais Obama anakwenda nchini humo 
wakati Mandela akiwa katika hali mbaya ya afya. Rais huyo wa zamani 
anatibiwa katika hospitali moja ya Pretoria.   
Alihamis rais Obama alisema ziara yake
 katika eneo ambalo watumwa wa Afrika waliondoka barani humo kwenda 
Amerika kaskazini imempa hamasa mpya ya kulinda haki za binadamu. 
Obama alitembelea kisiwa cha Goree 
kwenye ufukwe wa Senegal Alhamis.   Wanahistoria wanasema maelfu ya 
Waafrika wanaume kwa wanawake wakiwa wamefungwa minyororo walishikiliwa 
huko na kupitia kile kilichoitwa mlango wa kutorudi tena kupanda meli ya watumwa wakielekea bahari ya Atlantic.   
Rais Obama alisema ziara yake katika 
kisiwa hicho ilimpa hisia kali na nafasi ya kutathmini upya biashara ya 
utumwa katika karne ya 16 na 19. Chanzo: Voaswahili
No comments:
Post a Comment