TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, June 25, 2013

MMILIKI WA AC MILAN ATUPWA JELA MIAKA SABA KWA KUFANYA NGONO NA BINTI WA MOROCCO
italy4 440aa
Berlusconi ni mmiliki wa AC Milan, hapa akiwa katika picha ya pamoja na kocha wa zamani wa klabu hiyo, Carlo Ancelotti mwaka 2007
italy2 bfcf7
Binti wa Morocco, Karima El Mahroug
italy3 a5283
Rais wa Mahakama, Giulia Turri (katikati) akisoma hukumu
italy bac8b
Mwanasheria wa Silvio Berlusconi, Niccolo Ghedini akizungumza na Waandishi wa Habari nje ya Mahakama.
MMILIKI wa AC Milan, Silvio Berlusconi amehukumiwa kifungo cha miaka saba jela na kufungiwa maisha kufanya kazi katika ofisi za umma baada ya kukutwa na hatia ya kumlipa binti mdogo afanye naye ngono katika moja ya pati zake za 'bunga bunga'.
Waziri huyo Mkuu wa zamani wa Italia, Berlusconi, mwenye umri wa miaka 76, alimlipa binti mdogo wa Morocco, Karima El Mahroug, anayekwenda kwa jina la utani, Ruby, kwa ajili ya ngono na baadaye akajaribu kumbambikizia kesi ya wizi kwa kuwapigia simu Polisi na binti huyo akakamatwa. Berlusconi na mwanamke huyo wamekanusha kufanya ngono.
  
Mwendesha mashitaka alipendekeza afungwe miaka sita kwa kuzini ni binti mdogo na matumizi ya nguvu, lakini majaji watatu wa kike katika Mahakama ya Jijini Milan jana walitaka afungwe muda mrefu zaidi, miaka saba. 
Berlusconi pia amefungiwa maisha kufanya kazi katika ofisi za umma baada ya Waziri huyo Mkuu wa zamani kukutwa na hatia leo. 
Lakini mfungwa huyo anaweza kukata rufaa mara mbili kabla hajamaliza kifungo chake, ambayo inaweza kuchukua miezi au miaka.
  
Maana yake hatatumikia kifungo chake hadi ashindwe rufaa zake. 
Klabu yake ya AC Milan - ambayo amekuwa Rais wake kwa vipindi vitatu tofauti tangu mwaka 1987 - inayoundwa na nyota kadhaa akiwemo Mario Balotelli - ilimaliza katika nafasi ya tatu kwenye Ligi Kuu ya Italia, Serie A msimu uliopita ikizidiwa pointi 15 nyuma ya wapinzani, Juventus.
Baada ya hukumu, Mwanasheria wa Berlusconi, Niccolo Ghedini, mara moja alitangaza kukata rufaa akisema hukumu hiyo ni kama ilivyotarajiwa, haikutenda haki.
"Hii ni kinyume cha uhalisia," Ghedini aliwaambia Waandishi wa Habari nje ya Mahakama. "Nimetulia kwa sababu nimekuwa nikisema kwa miaka mitatu kwamba kesi haiwezi kuendeshwa hapa," alisema Ghedini. 

Kimwana: Karima el-Mahroug anafahamika kama 'Ruby the Heartbreaker'
Alisema pati hiyo ya chakula cha usiku ilikuwa kwa ajili ya watu maaum; Mwendesha mashitaka amesema walifanya ngono na mwanamke huyo aliyelipwa kuhudhuria.

Hata kama Berlusconi alikuwa anamjua mwanamke huyo katikati ya kesi hiyo, Karima el-Mahroug, anafahamika vyema kwa jina lake la utani, Ruby the Heart Breaker, ametoa ushahidi.

Alikuwa ana umri wa miaka 17 wakati huo anadaiwa kufanya kitendo hicho, lakini sasa amefikisha miaka 24. wakati umri wa kufanya ngono Italia ni miaka 14, na ni kinyume cha sheria kumlipa binti aliye chini ya umri wa miaka 18 kwa ajili ya ngono.

El-Mahroug aliitwa kwa utetezi, lakini akashindwa kutokea kwa sababu kadhaa,kuchelewesha hukumu. Timu ya Berlusconi mara moja ikamengua katika orodha ya mashahidi. Chanzo: AFP

No comments:

Post a Comment