TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, June 25, 2013

FELLAINI ATAKA PAUNI 100,000 KWA WIKI
article-2347673-18C30F23000005DC-982 634x4931 fa7ea
Marouane Fellaini anataka kujiunga na  Arsenal
KIUNGO Marouane Fellaini anataka kujiunga katika orodha ya wachezaji wanaolipwa Pauni 100,000 kwa wiki Arsenal, lakini The Gunners tayari imetenga dau kubwa kwa usajili mwingine.
Huku mshambuliaji wa Real Madrid, Gonzalo Higuain akiwa njiani kutua kwa dau la Pauni Milioni 22, The Gunners wataelekeza nguvu zao katika kuboresha safu ya kiungo.
 Fellaini ametokea kuwa mshindani mkuu wa nafasi mbele ya zoezi la Arsene Wenger kusaka kiungo, lakini dau kubwa linalotakiwa linaleta kama uhamisho huo utafanikiwa.
  Kutoka kikosi cha sasa cha Arsenal, ni Theo Walcott na Lukas Podolski peke yao wapo katika kiwango cha mshahara cha Pauni 100,000 kwa wiki.
 Mbali na kudai mshahara mkubwa, Arsenal pia watalazimika kufika bei anayouzwa Fellaini, Pauni Milioni 22- ambayo itafanya dili zima la usajili wake liendee kwenye Pauni Milioni 50. Chanzo: sportmail

No comments:

Post a Comment