TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, June 19, 2013

HISPANIA YATWAA UBINGWA U21 YAIBAMIZA ITALIA 4-2
2 a4e09
Hispania U-21 wakishangilia ubingwa baada ya kuibamiza Italia 4-2
3 a98b1
Hispania wakishangilia

1 0152d
Thiago Alcantara amefunga mabao matatu kipindi cha kwanza kuipa ushindi Hispania
4 2e457
5 badf3
  
6 30e65
KIUNGO Thiago Alcantara amekuwa kivutio katika ushindi wa kikosi cha vijana cha Hispania chini ya miaka 21 wa mabao 4-2 dhidi ya Italia na kutwaa Kombe la Ulaya kwa vijana barani humo, baada ya mchezaji huyo anayetakiwa na Manchester United kufunga mabao matatu mjini Jerusalem.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 wa Barcelona amekuwa akihusishwa kwa kiasi kikubwa na kuhamia Old Trafford.
Alcantara, aliyekuwamo kwenye kikosi cha Hispania kilichoshinda taji hilo miaka miwili iliyopita nchini Denmark, aliifungia timu yake bao la kwanza dakika ya sita, lakini Italia ikasawazisha haraka kupitia kwa Ciro Immobile dakika ya 10.
Thiago akafunga tena dakika ya 31 na 38 kwa penalti, kabla ya Isco kufunga dakika ya 66 kwa penalti pia na Borini akaifungia Italia dakika ya 79 kufanya 4-2.
Kikosi cha Hispania leo kilikuwa; De Gea, Montoya, Bartra, Martinez, Moreno, Koke/Camacho dk86, Illarramendi, Thiago, Tello/Muniain dk70, Morata/Rodrigo dk80 na Isco.
Italy U21; Bardi, Donati, Bianchetti, Caldirola, Regini, Florenzi/Saponara dk58, Rossi, Verratti/Crimi dk76, Insigne, Borini na Immobile/Gabbiadini dk58. Chanzo: sportmail

No comments:

Post a Comment