TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, June 4, 2013

MURINHO ATAKA WATANO KUIMARISHA CHELSEA 
KOCHA Jose Mourinho amewalenga wachezaji watano kuwasajili baada ya kurejea Chelsea kwa mara ya pili.
Wachezaji wa mwanzoni anaowataka wanafahamika ni washambuliaji wa Fiorentina, Stevan Jovetic, Manchester City, Edin Dzeko, sentahafu wa Porto, Eliaquim Mangala, Daniele De Rossi wa Roma na kiungo Mbrazil, Fernandinho wa Shakhtar Donetsk.
Mourinho pia ameweka wazi kumrejesha to Romelu Lukaku, baada ya kufanya vizuri msimu huu akiwa na West Brom ambako amefunga mabao 17, kwamba hataki atolewe kwa mkopo tena.
Kevin de Bruyne, ambaye ameomba kuuzwa moja kwa moja Borussia Dortmund baada ya kucheza kwa mkopo Werder Bremen, atakutana na kocha huyo mpya kabla ya kufikiwa uamuzi juu ya mustakabali wake.
Lakini Mourinho amesistiza hatafanya mabadiliko makubwa msimu huu.


1 35f4e
 
2 80619
 
4 672f9

5 9b4d8

No comments:

Post a Comment