TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, June 19, 2013

BRAZIL YAIBAMIZA MEXICO 2-0
brazil ab925
Neyman akishangilia baada ya kufunga bao
brzil2 56ec5
Wachezaji wa Brazil wakishangilia
brazil3 29006

brazil4 47cc4
Nayman akimtoka beki wa Mexico
brazil5 078fe
brazil6 5b4df
Shabiki wa Brazil
TIMU ya taifa ya Brazil imeshinda mechi yake ya pili ya Kombe la Mabara, huku kijana mdogo mwenye kipaji cha ajabu, Neymar akifunga bao tamu ndani ya dakika 10 za kwanza kabla ya kumtengenezea nafasi ya kufunga bao la pili Jo.
Brazil imeilaza Mexico mabao 2-0 bila ubishi na sasa inatimiza ponti sita na kuzidi kujiimarisha kileleni mwa Kundi A.
Daniel Alves alipinda krosi kutoka kulia na nyota mpya wa Barcelona, Neymar akaitokea wa kwanza mbele ya beki wa Mexico, kabla ya kuhadaa na kumtungua kipa Jose Corona dakika ya tisa na dakika ya 90 akampa pande Jo kufunga la pili.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Howard Webb wa Uingereza, kikosi cha Brazil kilikuwa: Cesar, Alves, Silva, Luiz, Marcelo, Luiz Gustavo, Paulinho, Oscar/Hernanes dk62, Hulk/Lucas Moura dk78, Neymar na Fred. 
Mexico: Corona, Rodriguez, Salcido,  Torrado, Dos Santos, Henandez, Moreno,  Guardado, Torres/Barrera dk70, Mier na Flores/Herrera dk68. 

No comments:

Post a Comment