TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, August 28, 2013

ZIMBABWE KUJENGA BUSTANI YA KIFAHARI

victoriafalls_6fed8.jpg
Serikali ya Zimbabwe imetangaza mpango wa kujenga kivutio cha kitalii, "Disneyland in Africa" katika maporomoko ya maji ya Victoria ili kuimarisha secta ya utalii nchini humo.
Waziri wa utalii wa Zimbabwe Walter Mzembi ameiambia BBC kuwa serikali ya nchi hiyo itatumia dola milioni mia tatu kujenga bustani hiyo.(P.T)
Serikali ya nchi hiyo inajaribu kufufua secta ya utalii iliyosambaratika kufuatia mzozo wa kisiasa uliodumu kwa takriban miaka kumi iliyopita na kushuka kwa dhamani ya safaru ya nchi hiyo.
Rais Robert Mugabe alichaguliwa kuhudumu kuwa rais wa nchi hiyo kwa muhula wa saba katika uchaguzi mkuu uliokamilika mwezi uliopita.
Lakini waziri huyo amesema, serikali yake haitategemea maporomoko hayo ya maji ya Victoria pekee, lakini amesema bwawa hilo linauwezo wa kuinua uchumi wa taifa hilo kwa kiasi kikubwa.
''Tunafikiria kuijenga bustani hiyo ili iwe sawa na bustani ya Disneyland nchini Marekani, na itajumuisha hoteli za kifahari, medani ya burudani, hoteli na vifaa vya kuandaa mikutano. Hii ndio maoni yetu na tunahitaji watu ambao wataweza kuiendesha'' Alisema waziri huyo.
Awali Mzembi aliliambia shirika la habari la serikali la nchi hiyo kwua serikali ya rais Robert Mugabe inadhamiria kuanzisha mfumo ambao utaruhusu soko huria katika secta ya mabenki nchini humo, ambapo watu ambao sio raia wa nchi hiyo wanaweza kufungua akaunti nchini humo.
Waziri huyo aliyasema hayo wakati wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu utalii unaoandaliwa kwa pamoja na Zimbabwe na Zambia.
Uamuzi huo wa kuipa Zimbabwe fursa ya kuandaa kongamano hilo la Umoja wa Mataifa, umeshutumiwa vikali na shirika la kutetea haki za kibinadam la Umoja huo, lililo na makao yake mjini Geneva, likadai serikali ya nchi hiyo inaendelea kukiuka haki za kibinadam na kuwa uchaguzi uliokamilika hivi majuzi haukuwa huru na wa haki.
Serikali ya Zimbabwe pia inapanga kupanua uwanja wa Ndege wa Victoria Fall, mradi ambao utagharimu dola milioni mia moja hamsini.
Katika kipindi cha miezi mitatu ya kwanza mwaka huu, secta ya utalii nchini humo ilikuwa kwa asilimia kumi na saba na ikiwa uthabiti wa taifa hilo utadumishwa secta ya utalii ina uwezo wa kuchangia pato la taifa hilo kwa asilimia kumi na tano.

No comments:

Post a Comment