SAMUEL ETO'O ATAMBULISHWA RASMI CHELSEA

Chelsea imemsajili mshambuliaji wa Cameroon, Samuel Eto'o kutoka klabu ya Anzi Makhachkala ya Urussi.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka thelathini na miwili amesaini mkataba wa mwaka mmoja na Chelsea.
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho, 
aliamua kumsajili Eto'o baada ya maombi yake ya kumsajili nyota wa 
Manchester United Wayne Rooney kukataliwa.(P.T)

Mapema 
wiki hii, ilibainika kuwa Rooney hakuwa tayari kulazimisha uhamisho wake
 kwa kuwasilisha ombi lake la kutaka kuondoka na hivyo kuzima matumaini 
ya Chelsea ya Kumsajili mchezaji huyo.
Mchezaji huyo ambaye ni mshindi mara 
nne wa mchezaji bora wa soka barani Afrika, alikuwa nyota wa AC Milan 
mwaka wa 2010 wakati Mourinho alipoiongoza kushinda kombe la klabu 
bingwa barani Ulaya.
Mwaka wa 2011, Eto'o alivunja rekodi ya kuwa mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa zaidi duniani.
Klabu hiyo ya Anzi pia imemuuza kiungo
 wake Willian, mwenye umri wa miaka 25 kwa klabu ya Chelsea, baada ya 
mmiliki wa klabu hiyo mfanya biashara tajii Suleyman Kerimov kupunguza 
bajeti ya klabu hiyo.

Eto'o
 alianza kucheza soka ya kulipwa na klabu ya Real Madrid, lakini 
alisajiliwa na vilabu vya Leganes na Real Mollorca kwa mkopo kabla ya 
kupata mkataba wa kudumu Mallorca mwaka wa tisini na tisa.
Mchezaji huyo ambaye alikuwa katika 
kikosi cha Cameroon kilichoshinda kombe la mataifa ya Afrika mwaka wa 
2002, vile vile alishinda kombe la Copa del Rey, kabla ya kujiunga na 
klabu ya Barcelona mwaka wa 2004.
Akiwa katika uwanja wa Nou Camp, 
alishinda kombe la klabu bingwa barani ulaya mara mbili mwaka wa 2006 na
 2009 na alifunga bao katika fainali hizo mbili pamoja na kushinda kombe
 la ligi kuu ya La Liga mara tatu.
Mwaka wa 20098, Barcelona iliilipa 
Inter Milan pauni milioni arubaini pamoja na mchezaji huyo ili kumsajili
 Zlatan Ibrahimovic na mshambuliaji huyo alifanikiwa kushinda kombe la 
klabu bingwa barani Ulaya kwa mara nyingine chini ya Uongozi wa Mourinho
 katika uwanja wa San Siro.
Alijiunga na klabu ya Anzi na ripoti zinasema kuwa alikuwa akilipwa £167,825 kwa wiki mwaka wa 2011.
No comments:
Post a Comment