TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, August 28, 2013

MAJANGA ARSENAL, PODOLSKI NJE SIKU 21, RAMSEY NA WILSHERE NAO WAUMIA

10 74adc
Lukas Podolski ameongeza idadi ya majeruhi Arsenal na chini akitolewa uwanjani jana (HM)

20 d00eb
Jack Wilshere aliumia kifundo cha mguu, lakini akaendelea na mechi Arsenal ikiifunga Fenerbahce
30 8c787
Aaron Ramsey aliondoka uwanjani kabla ya mwisho wa mechi kutokana na maumivu ya nyonga
MSHAMBULIAJI wa Arsenal, Lukas Podolski ataukosa mchezo wa Jumapili wa wapinzani wa London Kaskazini, dhidi ya Tottenham baada ya kuumia nyama katika mchezo wa Ligi ya Mabinwa jana dhidi ya Fenerbahce.
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ujerymani anatarajiwa kuwa nje ya Uwanja kwa wiki tatu baada ya kuumia katika dakika za mwanzoni za kipindi cha pili kwenye ushindi wa 2-0 katika mchezo huo wa marudiani, hivyo timu yake kusonga mbele hatua ya makundi kwa ushindi wa jumla wa 5-0 dhidi ya Waturuki.
Kocha Arsene Wenger amesema: "Tmetugharimu mno kwa majeruhi hayo, kwa sababu tunampoteza Podolski.
Aaron Ramsey alifunga mabao yote katika usiku huo Arsenal ikijikatia tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa kwa mara ya 16 mfululizo.
Lakini mchezaji huyo wa kimataifa wa Wales naye pia alikuwa miongoni mwa wachezaji walioumia, akitoka nje kabla ya mwisho wa mchezo na kuiacha Gunners ikimalizia mechi na wachezaji 10.
Kiungo Jack Wilshere pia naye alipatwa na misukosuko, alipokabiliana na Raul Mereiles na Bruno Alves, na kumuachia maumivu.
Wenger alisema: "Sifahamu kiasi gani Ramsey ameumia. Sifahamu Wilshere anaendeleaje. Tutaangalia hiyo kesho (leo) asubuhi. Makwanja mawili kwa Wilshere yalisikitisha, lakini anaonekana yuko sawa.
"Jack atakuwa sawa Jumapili. Natumai hivyo kwa Aaron pia. Nilimuona akitoka nje zikiwa zimesalia dakika tatu au nne mechi kumalizika, lakini sijui anajisikia vibaya kiasi gani. Alitaka kubaki uwanjani,".
Wenger alitaka kumtoa nje Wilshere, kutokana na historia ya matatizo ya maumivu ya kifundo cha mguu kwa mchezaji huyo, lakini mchezaji huyo akaamua kuendelea kucheza.
"Nilitaka kumtoa nje, ndiyo," Wenger alisema. Chanzo: binzubeiry

No comments:

Post a Comment