TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Saturday, August 17, 2013

ANC YASUSIA IBADA YA MARIKANA mine-shootings-reaction-horizontal-large-gallery 4e56f

Maelfu ya raia wa Afrika Kusini wamekusanyika katika mgodi mkubwa wa dhahabu nyeupe kuadhimisha mwaka mmoja tangu kuuawa kwa wachimba migozi 34. Chama tawala cha ANC kimesema hakitahudhuria makumbusho ya leo kikisenya yanatumiwa kukejeli utawala wa nchi.
P.T
Katika maadhimisho hayo Afisa mtendaji wa kampuni ya, Lonmin, Ben Magara amwaomba mshamaha familia za wachimba migodi 34 waliouawa.
Tofauti kati ya makundi mawili ya vyama vya wafanyikazi zililaumiwa kwa kuzuka vurugu zilizotokea mwaka jana.Chama kilicho na uhusiano wa karibu na ANC- National Union Of Mineworkers kimepingwa na wachimba migodi wengi na kuanzisha chama kipya. Mauaji hayo yalisababisha gathabu ya umma na kupelekea lalama nyingi dhidi ya sekta ya madini.
Afrika Kusini ina asili mia 80 ya madini ya dhahabu na dhahabu nyeupe.Mauaji ya wafanyikazi hao yalitajwa kuwa mabaya zaidi tangu kumalizika kwa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini mwaka 1994. Sherehe za leo zimepangwa na chama kipya cha kutetea maslahi ya wachimba migodi Mineworkers and Construction Union (Amcu) ambacho kinashinikiza nyongeza zaidi ya marupurupu ya wafanyikazi.
AMCU ndicho kikubwa zaidi katika mgodi wa dhahabu nyeupe inayomilikiwa na kampuni ya Lonmin.Baadhi katika chama tawala cha ANC wameelezea hofu huenda chama hicho kikaungana na aliyekua kiongozi wa vijana Julius Malema ambaye alifukuzwa chamani kwa makosa ya nidhamu.
Malema ameunda chama chake cha kisiasa. Rais Jacob Zuma aliunda tume ya kuchuguza matukio yaliyopelekea mauaji ya wachimba migodi hio. Mwandishi wa BBC Afrika Kusini anasema kumekuwa na ghathabu ya umma kwani hadi sasa hakuna polisi hata mmoja aliyewajibishwa na mauaji hayo.

No comments:

Post a Comment