KIJANA ALIYEKAMATWA NA MWAKYEMBE 
Siku moja baada ya ziara ya kushtukiza
 ya waziri wa uchukuzi Dk. Harison Mwakyembe, kwenye uwanja wa ndege wa 
kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar-es-Salaam, kiasi kikubwa cha dawa
 za kulevya kimekamatwa uwanjani hapo katika harakati za kusafirishwa 
kwenda nchi za nje.

Waziri wa
 Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akionesha picha ya kijana Leonard 
Jeremiah Monyo ( Edwin Jeremiah Monyo) ambaye amekamatwa na kete 86 za 
madawa ya kulevya aina ya heroine
Juhudi za Dk. Mwakyembe na Dawa za Kulevya, Amnasa Rasta Akisafirisha Madawa Uwanja wa JNIA Dar es Salaam
JUHUDI za Waziri wa Uchukuzi, Dk. 
Harrison Mwakyembe za kupambana na dawa za kulevya nchini Tanzana 
zimeanza kuzaa matunda baada ya jana akiwa katika ukaguzi wa Kiwanja cha
 Ndege cha Kimataifa Julius Nyerere kunaswa kijana akijaribu kupita na 
dawa za kulevya katika uwanja huo.
Kwa kile kuoneshwa kukerwa na tabia 
hizo, Dk. Mwakyembe amempiga picha kijana huyo ambaye ni rasta na pita 
yake itasambazwa maeneo tofauti, huku kesi yake ikiendelea ya kupatikana
 na madawa hayo ya kulevya.
Akizungumza na vyombo vya habari leo 
ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Dk. Mwakyembe alimtaja kijana 
aliyekamatwa jana kuwa ni Leonard Jeremiah Monyo (Edwin Jeremiah Monyo) 
ambaye amekamatwa na kete 86 za madawa ya kulevya aina ya heroin akitaka
 kusafiri nazo kuelekea misokoto ya bangi 34 akiwa ameficha kwenye begi 
lake.
Alisema kijana huyo rasta alinaswa na 
mtambo wa kukagua mzigo baada ya wakaguzi kuushuku mzigo wake hivyo 
kuamuru ukaguliwe ndipo alipokutwa na madawa hayo haramu akijaribu 
kusafiri nayo kwa ndege.
Alisema kijana huyo kwa sasa 
anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa uchunguzi zaidi kabla ya kufikishwa 
mahakamani kujibu mashtaka ya kukutwa na dawa hizo haramu. Alisema kwa 
kile kuoneshwa kukerwa na vitendo hivyo na kuamua kwa dhati kupambana 
navyo wamempiga picha kijana huyo na picha zake zitasambazwa maeneo 
mbalimbali ili aonekane na umma kujua watua ambao wamekuwa wakilichafua 
taifa nje na ndani kutokana na biashara hizo haramu.
Dk. Mwakyembe amesema atahakikisha 
anafuatilia kesi ya kijana huyo hadi itakapoishia ili uona hatua za 
kisheria zinachukuliwa kwa wahusika na vitendo hivyo kukomeshwa. Alisema
 maofisa wakaguzi wa mizigo wawili (wote wasichana) ambao walimnasa 
kijana huyo watazawadiwa na kupandishwa daraja kutokana na kazi nzuri 
waliyoifanya.
"Jana tu baada ya ukaguzi wenzetu 
ambao wanaona kama tunafanya mzaha jana tena wakapitisha mzigo wa madawa
 ya kulevya kiwanja cha ndege cha Dar es Salaam, kwa sababu vijana wetu 
sasa wameamka na hawataki mchezo wakamkamata kijana huyo...," alisema.
"Picha yake itasambazwa kila 
sehemu...sidhani kama tunahitaji upelelezi kwa sababu tumekukamata na 
dawa za kulevya. Mimi na viongozi wangu kupitisha dawa za kulevya 
akikisha kuuhakikisha.
Alisema kijana huyo alikamatwa majira 
ya saa mbili na nusu usiku akiwa anasafiri kwenda nchini Italia kwa 
kutumia ndege ya kampuni ya Swissair. Alisema kwa sasa kila 
atakayekamatwa na dawa za kulevya picha yake itasambazwa maeneo 
mbalimbali ya nchi ili watu hao wajulikane.
Alisema kwa sasa taratibu zinafanywa 
ili kuhakikisha mizigo ya abiria wanaowasili kutoka nje ya nchi kuingia 
Tanzania nao mizigo ikaguliwe ili kuwabaini wanaoingiza bidhaa hiyo 
haramu ichini pia. Aliongeza zoezi hilo litafanyika katika viwanja vya 
ndege na bandarini kwa kila mizigo inapowasili.
Alisema lengo ni kuhakikisha viwanja 
vya ndege vinakuwa salama na kuacha kutumika vibaya na baadhi ya watu, 
jambo ambalo limeendelea kulichafua taifa. Alisem kiwanja cha Dar es 
Salaam ni kizuri na kina vifaa vya usalama vya kutosha ila mapungufu 
yaliyopo ni kwa baadhi ya wafanyakazi ambao wanatumia vibaya madaraka 
yao.
Dk. Mwakyembe ameahidi kuwataja na 
kuweka picha zao hadharani watu ambao wanajihusisha na madawa hayo ya 
kulevya. Amesema wanatarajia kutaja majina ya Watanzania ambao hivi 
karibuni walinaswa na dawa za kulevya nchini Afrika Kusini katika uwanja
 wa ndege wa Oliver Tambo. Alisema Watanzania wengine wamekamatwa Hong 
Kong wakihusishwa na dawa hizo na wanafuatilia pia picha na majina yao 
yatawekwa hadharani muda wowote.
*Imeandaliwa na www.thehabari.com
No comments:
Post a Comment