Unicef : Dola za Marekani Milioni 500 zahitajika Iraq

Mpiganaji wa Islamic State akibebelea bendera ya kundi lake, karibu na mpaka wa Iraq na Syria.
Na RFI
Mashirika
 mbalibali ya kibinadamu yanapanga kuzindua mchango wa kutafuta Dola za 
Marekani Milioni 500 kukabiliana na hasara iliyosabishwa na wapiganaji 
wa Islamic State nchini Iraq.
Mchango huu unasimamiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maswala ya watoto Unicef.
Mwakilishi
 wa Unicef nchini Iraq Philippe Heffinck, amesema hali ya kibainadamu 
nchini humo ni mbaya sana na shirika hilo linahitaji fedha hizo ili 
kuendelea kuwasaidia zaidi ya watu Milioni 8 waliothirika.
Haya 
yanajiri wakati huu Marekania ikijiandaa kuwa mwenyeji wa mkutano wa 
kimataifa jijini Paris nchini Ufaransa kujadili namna ya kuendeleka 
kukabiliana na Islamic State nchini Iraq na Syria.(P.T)
No comments:
Post a Comment