TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, June 14, 2015

SERIKALI NA WADAU WA MAENDELEO WATAKIWA KUFUATA HAKI ZA BINADAMU

index
Mahmoud Ahmad Arusha
Serikali na wadau wa maendeleo wametakiwa kuzingatia usawa,haki,sheria ilikutimiza wajibu wao wa kutoa huduma kwa jamii yenye ulemavu wa ngozi sawa na kufuata haki za binadamu ili kufikia malengo ya milenia.
Kauli hiyo imetolewa na mkurugenzi mkazi wa umoja wa mataifa hapa nchini Alvaro Rodrigues wakati akizungumza kwenye maadhimisho ya kilele cha siku ya walemavu duniani yaliofanyika kitaifa mkoani hapa.
Rodrigues alisema kuwa tunaposherehekea siku hiyo ya kupata ufahamu juu ya watu wa jamii yenye ulemavu wa ngozi(ALBINO)tunawaji kujua kuwa jamii hiyo inahitaji nini na je mahitaji yao yanapatikana ikiwemo kupewa ulinzi wa maisha yao kama usawa,haki na sheria.
Alisema kuwa Angependa kuzungumzia mambo makubwa matatu yatakayo wakumbusha jamii kwa kuwa ni kweli kuna maendeleo katika kuboresha haki za binadamu hapa nchini katika makundi yote hivyo umoja huo ulikishirikiana na serikali na wadau wa maendeleo utambue wajibu wao kwa watu wa jamii hiyo kwani hiyo ni moja kati ya haki za binadamu.
Aidha aliwataka kufanyaikazi kwa nia ya dhati na kuzuia na kukomesha ukatili dhidi yao kwa watu wenye ulemavu wa ngozi bila kusahau kuwa watu wa jamii hiyo wamekuwa hawana uwezo wa kumudu gharama mbalimbali zikiwemo dawa,hivyo wapewe kipaumbele kwani ni haki yao ya kimsingi.
“Umoja wa mataifa unaendelea kufanyakazi kwa pamoja na serikali na jamiii kwa ujumla kuboresha utawala wa sheria katika kila mwelekeo pamoja na watu wenye ulemavu wa ngozi hapa lazima tuipongeze serikali kwa kufuatilia kwa ukaribu mauaji ya jamii hii ila tuwapende tuwatunze kwani binadamu waote ni sawa”alisema Rodrigues
Nao jumuiya ya ulaya katika taarifa yao kwa vyombo vya habari wamaepinga mauaji ya jamii hiyo na kuitaka serikali kuchukua hatua stahiki kuwalinda na kuheshimu haki za binadamu kwa kuwapatia mahitaji stahiki jamii hiyo kwani imekuwa inakumbana na changamoto kubwa katika maisha yao ya kila siku.
Kwa upande wake raisi wa taasisi ya social Protection Association Hassan Abdulrahman alisema kuwa wao wameandaa Bonanza la kupinga mauaji ya albino litakalofanyika jijini Dar es salaam sanjari na kongamano kwa wanafunzi wa vyuo 10 mkoani humu.
Alisema kuwa hiyo yote ni katika kuahakikisha masuala ya mauaji ya watu wenye ulemavu hapa nchi yanakuwa historian a watu wanajali haki za binadamu wenzao kwani ukatili huo unatisha na unawanyima haki yao ya kuishi.
Alisema wanatarajia kwa kila chuo kuwafikia wanafnzi zaidi ya mia mbili na baadae kutoa elimu kwa jamii ya watanzania wote kufahamu madhila wanayopata wenzao katika maisha yaoa ya kila siku na kuwa bonanza na kongamano vitafanyika mwishoni mwa mwezi huo na mwezi ujao.
Wakati huo huo umoaj wa waganga wa jadi hapa nchi umepinga vikali sula la upigaji ramli kwa waganga wa jadi katika kuhakikisha dhana potofu ya kuwa viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi vinaleta utajiri.
Akizungumza na gazeti hili Mratibu wa umoja huo Julius Juju alisema kuwa changamoto kubwa wanayokumbana nao kwenye majukumu ya kazi yao ni upigaji wa ramli nah ii ndiyo sababu kubwa inayopelekea mauji hayo nao wanayapinga kwa nguvu zao na kuwa watashirikiana na serikali kwa ukaribu kuhakikisha wale wote wenye dhna potofu wanaingia kwenye mikono ya serikali.
Akatanabaisha kuwa wamekuwa wakipata changamoto kutoka kwa waratibu wa afya wa serikali ambao wamekuwa wakichelewesha ushirikiano wao na serikali katika kufikia malengo na kuondoa tatizo wao wanapinga mauaji hayo wakiamini viungo vya Albino haviwezi kuwapatia wananchi utajiri.
“Hapa ikumbukwe kuwa kutetea hai za binadamu wengi sanjari na uedeshaji wa kupiga ramli ndio changamoto kubwa katika mauaji ya jamii sisi kama uwawa tunapinga mauaji na tunapenda kutambulika kisheria katika serikali yetu na tutatoa ushirikiano kuhakikisha wenzetu wachache wanaotuchafua sheria inachukuwa mkondo wake”alisisitiza Juju.(Muro)

No comments:

Post a Comment