Miili 23 ya ajali ya basi la Another G na lori Mufindi Iringa yatambuliwa
Mkuu wa 
wilaya ya Mufindi mkoani Iringa Bi Mboni Mhita (kushoto)  akiwa na 
wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya hiyo ya Mufindi katika 
kuwatembelea wagonjwa katika Hospitali ya  wilaya ya Mufindi.
Baadhi ya ndugu wakichukua mwili wa ndugu yao baada ya kuutambua
Mkuu  wa 
wilaya ya  Mufindi Bi Mboni Mhita (kushoto)  akimfariji mmoja kati ya 
majeruhi wa ajali ya  basi la Another G na lori  iliyoua 23 na kujeruhi 
34 jana, wengine pichani ni wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama 
wilaya ya  Mufindi (picha na matukiodaimaBlog).(DK)
        
*DC Mhita awashauri TBS kukagua ubora wa vyombo vya usafiri
MIILI 
yote  23 ya ajali  ya basi  aina Coaster mali ya kampuni ya  Another G 
lenye  namba  za  usajili  T 927 CEF aina ya  mitsubishi fuso iliyokuw3a
 ikifanya  safari  zake  kati ya Iringa – Njombe ambalo  liligoganga na 
uso kwa  uso na lori lenye namba za usajili T 916AQM  likiwa na  Tela 
lenye namba za usajili T 965 BEH Scania imetambuliwa na  ndugu  zao.
Kwa 
mujibu wa Mkuu  wa wilaya ya Mufindi ambae ni mwenyekiti wa kamati ya 
ulinzi na usalama ya  wilaya Bi Mboni Mhita kuwa ndugu wa marehemu  hao 
 waliokufa katika ajali  waliweza  kutambua  miili ya ndugu zao jana na 
leo na kuwa hadi  sasa hakuna mwili ambao bado kutambulia na  hivyo 
kuvishukuru  vyombo  vya habari kwa kushiriki kuhabarisha  juu ya ajali 
 hiyo  na wananchi  ambao  waliitikia na kufika kutambua miili hiyo.
Akizungumza
 na  mtandao huu wa www.matukiodaima.co.tz Mkuu  huyo wa wilaya Bi 
Mboni  alisema  kuwa  jitihada  kubwa zimeonyeshwa na  vyombo  vya 
habari  vya ndani ya mkoa  wa Iringa na nje ya  mkoa ikiwemo mitandao 
ya  kijamii katika kuhabarisha  umma na ndio  sababu ya utambuzi  wa 
miili hiyo kufanikiwa mapema baada ya habari kuenezwa vilivyo.
Pia  
mkuu  huyo wa wilaya   alipongeza  uongozi  wa JKT Mafinga  na uongozi  
wa kitaifa  wa jeshi   hilo kwa  kujitolea  kusaidia mazishi ya vijana 
wake  ambao walikuwa wakielekea JKT Mafinga kwa ajili ya  kuripoti kwa 
kuanza mafunzo ya jeshi na baadhi yao  kufa katika ajali hiyo huku 
baadhi  wakijeruhiwa kwani alisema ni vigumu kwa taasisi kujitolea  
kusaidia mtu ambae hana mkataba nae.
Aidha  
mkuu  huyo  wa  wilaya aliwaomba  wananchi wote  nchini ambao ndugu  zao
 walipoteza maisha katika ajali ya basi la Majinja lililoua watu  zaidi 
ya 50 katika  eneo la Changalawe  mjini Mafinga  kufika kituo cha  
polisi Mafinga kwa ajili ya kutambua  na kuchukua mizigo ya  ndugu zao  
waliopoteza maisha katika ajali hiyo na kuwa mali  zote za marehemu hao 
zimehifadhiwa salama.
Hata  
hivyo  mkuu  huyo  wa  wilaya ya  Mufindi Bi Mboni alivitaka vyombo  vya
 usalama  barabarani katika  wilaya ya Mufindi  kuendelea na mkakati  
wake wa  kuwabana madereva wanaovunja  sheria  za  barabarani na 
kuwachukulia hatu kali kama  njia ya  kupunguza ajali  hiyo.
Alisema 
askari  hao  pia  wanapaswa  kukagua ubora  wa  vyombo  vya usafiri 
vyote na  vile ambavyo havina  ubora  ni heri  kuvifungia  hadi 
vitakapoboreshwa  kuliko  kuruhusu vyombo  vya  usafiri  chakavu  
kufanya kazi  ya usafirishaji  wa abiria .
Kuhusiana
 na wajibu  wa  shirika la viwango Tanzania (TBS) mkuu  huyo wa wilaya 
alishauri kuwepo na mkakati makini wa TBS  kukagua  ubora  wa vyombo  
vya usafiri vinavyoingizwa  nchini kwani mabasi  mengi ya abiria siti 
zake zimeshikiliwa na ngundi ya mbao na baada ya kutokea ajali siti hizo
 hung’ooka na kama abiria amefunga mkanda hulazimika kuchomoka na siti 
yake .
Alisema 
katika ripoti ya ajali ya kwanza ya basi la Majinja  iliyotokea Machi 
mwaka huu na kuua watu zaidi ya 50 kamati ya uchunguzi  ilibainihilona 
kuwa mwenye uwezo wa  kukagua  viwango  vya vyombo  hivyo vya usafiri ni
 TBS kwa kushirikiana na wadau wengine kama Sumatra na jeshi la polisi  
kupitia kitengo  cha usalama barabarani.
Wakati  
serikali ya  wilaya ya  Mufindi kupitia mkuu  huyo wa  wilaya ikishauri 
TBS na  washirika  wake  kuweka mkakati wa kukagua   viwango  vya 
vyombo   hivyo  vya usafiri baadhi ya  wananchi   wilaya ya  Mufindi na 
mkoa wa Iringa wamekuwa na maoni  tofauti kwa  kulitaka jeshi la polisi 
kitendo  cha askari wa usalama barabarani kuanza kusindikiza mabasi hayo
 yanayotoka  usiku mkoani Njombe na Iringa ili  kuhakikisha abiria   
hawazidi katika mabasi hayo ya usiku.
Zacharia 
Sanga  mkazi  wa Mafinga  wilaya ya Mufindi na John Lumwesa mkazi  wa 
Iringa mjini  walisema kuwa  kimsingi mabasi hayo  yanajaza  abiria  
kupita  kiasi na kutembea kwa mwendo mkali  zaidi kutokana na nyakati za
 usiku  askari  wa usalama barabara  kutokuwepo.
Hivyo 
walitaka askari wa usalama barabarani kuendelea kuwepo na tochi hadi 
usiku ili kuthibiti ajali mbaya kama  hiyo ambayo mbali ya  kuwa ni 
uzembe wa dereva  wa basi ila kukosekana kwa askari  wa usalama 
barabarani  usiku ni  moja ya  sababu.
Mganga 
Mkuu  wa Hospitali ya wilaya ya Mufindi Dr  Godluck  Mlimbila  alisema  
kuwa hali za majeruhi 34 waliokuwa  wamelazwa katika  Hospitali hiyo 
zinaendelea  vizuri na  kuwa mbali ya  wale  wanne ambao  hali  zao 
zilikuwa mbaya  zaidi na kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa
 Iringa katika Hospitali  hiyo hadi jana majira ya saa 8 mchana  ni 
majeruhi kati ya 8 na 10  pekee  ndio ambao  walikuwa  wakiendelea na 
matibabu huku  wengi  wao wakiwa  wameruhusiwa baada ya hali  zao 
kuendelea vema .
No comments:
Post a Comment