TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, June 16, 2015

Miili 23 ya ajali ya basi la Another G na lori Mufindi Iringa yatambuliwa


Mkuu wa wilaya ya Mufindi mkoani Iringa Bi Mboni Mhita (kushoto)  akiwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya hiyo ya Mufindi katika kuwatembelea wagonjwa katika Hospitali ya  wilaya ya Mufindi.

Baadhi ya ndugu wakichukua mwili wa ndugu yao baada ya kuutambua

Mkuu  wa wilaya ya  Mufindi Bi Mboni Mhita (kushoto)  akimfariji mmoja kati ya majeruhi wa ajali ya  basi la Another G na lori  iliyoua 23 na kujeruhi 34 jana, wengine pichani ni wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya  Mufindi (picha na matukiodaimaBlog).(DK)
*DC Mhita awashauri TBS kukagua ubora wa vyombo vya usafiri
MIILI yote  23 ya ajali  ya basi  aina Coaster mali ya kampuni ya  Another G lenye  namba  za  usajili  T 927 CEF aina ya  mitsubishi fuso iliyokuw3a ikifanya  safari  zake  kati ya Iringa – Njombe ambalo  liligoganga na uso kwa  uso na lori lenye namba za usajili T 916AQM  likiwa na  Tela lenye namba za usajili T 965 BEH Scania imetambuliwa na  ndugu  zao.
Kwa mujibu wa Mkuu  wa wilaya ya Mufindi ambae ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya  wilaya Bi Mboni Mhita kuwa ndugu wa marehemu  hao  waliokufa katika ajali  waliweza  kutambua  miili ya ndugu zao jana na leo na kuwa hadi  sasa hakuna mwili ambao bado kutambulia na  hivyo kuvishukuru  vyombo  vya habari kwa kushiriki kuhabarisha  juu ya ajali  hiyo  na wananchi  ambao  waliitikia na kufika kutambua miili hiyo.
Akizungumza na  mtandao huu wa www.matukiodaima.co.tz Mkuu  huyo wa wilaya Bi Mboni  alisema  kuwa  jitihada  kubwa zimeonyeshwa na  vyombo  vya habari  vya ndani ya mkoa  wa Iringa na nje ya  mkoa ikiwemo mitandao ya  kijamii katika kuhabarisha  umma na ndio  sababu ya utambuzi  wa miili hiyo kufanikiwa mapema baada ya habari kuenezwa vilivyo.
Pia  mkuu  huyo wa wilaya   alipongeza  uongozi  wa JKT Mafinga  na uongozi  wa kitaifa  wa jeshi   hilo kwa  kujitolea  kusaidia mazishi ya vijana wake  ambao walikuwa wakielekea JKT Mafinga kwa ajili ya  kuripoti kwa kuanza mafunzo ya jeshi na baadhi yao  kufa katika ajali hiyo huku baadhi  wakijeruhiwa kwani alisema ni vigumu kwa taasisi kujitolea  kusaidia mtu ambae hana mkataba nae.
Aidha  mkuu  huyo  wa  wilaya aliwaomba  wananchi wote  nchini ambao ndugu  zao walipoteza maisha katika ajali ya basi la Majinja lililoua watu  zaidi ya 50 katika  eneo la Changalawe  mjini Mafinga  kufika kituo cha  polisi Mafinga kwa ajili ya kutambua  na kuchukua mizigo ya  ndugu zao  waliopoteza maisha katika ajali hiyo na kuwa mali  zote za marehemu hao zimehifadhiwa salama.
Hata  hivyo  mkuu  huyo  wa  wilaya ya  Mufindi Bi Mboni alivitaka vyombo  vya usalama  barabarani katika  wilaya ya Mufindi  kuendelea na mkakati  wake wa  kuwabana madereva wanaovunja  sheria  za  barabarani na kuwachukulia hatu kali kama  njia ya  kupunguza ajali  hiyo.
Alisema askari  hao  pia  wanapaswa  kukagua ubora  wa  vyombo  vya usafiri vyote na  vile ambavyo havina  ubora  ni heri  kuvifungia  hadi vitakapoboreshwa  kuliko  kuruhusu vyombo  vya  usafiri  chakavu  kufanya kazi  ya usafirishaji  wa abiria .
Kuhusiana na wajibu  wa  shirika la viwango Tanzania (TBS) mkuu  huyo wa wilaya alishauri kuwepo na mkakati makini wa TBS  kukagua  ubora  wa vyombo  vya usafiri vinavyoingizwa  nchini kwani mabasi  mengi ya abiria siti zake zimeshikiliwa na ngundi ya mbao na baada ya kutokea ajali siti hizo hung’ooka na kama abiria amefunga mkanda hulazimika kuchomoka na siti yake .
Alisema katika ripoti ya ajali ya kwanza ya basi la Majinja  iliyotokea Machi mwaka huu na kuua watu zaidi ya 50 kamati ya uchunguzi  ilibainihilona kuwa mwenye uwezo wa  kukagua  viwango  vya vyombo  hivyo vya usafiri ni TBS kwa kushirikiana na wadau wengine kama Sumatra na jeshi la polisi  kupitia kitengo  cha usalama barabarani.
Wakati  serikali ya  wilaya ya  Mufindi kupitia mkuu  huyo wa  wilaya ikishauri TBS na  washirika  wake  kuweka mkakati wa kukagua   viwango  vya vyombo   hivyo  vya usafiri baadhi ya  wananchi   wilaya ya  Mufindi na mkoa wa Iringa wamekuwa na maoni  tofauti kwa  kulitaka jeshi la polisi kitendo  cha askari wa usalama barabarani kuanza kusindikiza mabasi hayo yanayotoka  usiku mkoani Njombe na Iringa ili  kuhakikisha abiria   hawazidi katika mabasi hayo ya usiku.
Zacharia Sanga  mkazi  wa Mafinga  wilaya ya Mufindi na John Lumwesa mkazi  wa Iringa mjini  walisema kuwa  kimsingi mabasi hayo  yanajaza  abiria  kupita  kiasi na kutembea kwa mwendo mkali  zaidi kutokana na nyakati za usiku  askari  wa usalama barabara  kutokuwepo.
Hivyo walitaka askari wa usalama barabarani kuendelea kuwepo na tochi hadi usiku ili kuthibiti ajali mbaya kama  hiyo ambayo mbali ya  kuwa ni uzembe wa dereva  wa basi ila kukosekana kwa askari  wa usalama barabarani  usiku ni  moja ya  sababu.
Mganga Mkuu  wa Hospitali ya wilaya ya Mufindi Dr  Godluck  Mlimbila  alisema  kuwa hali za majeruhi 34 waliokuwa  wamelazwa katika  Hospitali hiyo zinaendelea  vizuri na  kuwa mbali ya  wale  wanne ambao  hali  zao zilikuwa mbaya  zaidi na kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa katika Hospitali  hiyo hadi jana majira ya saa 8 mchana  ni majeruhi kati ya 8 na 10  pekee  ndio ambao  walikuwa  wakiendelea na matibabu huku  wengi  wao wakiwa  wameruhusiwa baada ya hali  zao kuendelea vema .

No comments:

Post a Comment