TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, June 16, 2015

DJ Khaled kumbe anaogopa kusafiri kwa ndege !! Kisa ni hiki alichosema hapa..

dddddjjj
Producer, Rapper na DJ wa muziki Marekani, Dj Khaled siku chache zilizopita alikuwa kwenye Interview moja ya Radio ndani ya Los Angeles, Marekani.
Kati ya mambo waliyoongelea kuna kitu kimoja nimekijua baada ya kumsikia kwenye Interview hiyo… DJ Khaled aliulizwa kwa nini hapendi kutumia usafiri wa ndege>>>“…aah bwana mimi ndege zinanipa presha, sio utani, pale ndege inapoanza kuondoka uwanjani kuna ule muungurumo na mtikisiko wa ndege inapoanza kupaa… ile mimi inanipa tumbo joto yani hua napanic, natoa jasho natetemeka na vitu kama hivyo yani!! kibaya zaidi unakuta Pilot wa ndege anatoa tangazo kua hali ya hewa itakua mbaya safari nzima! Hapo inamaanisha safari nzima tutakua tumeshikilia roho zetu mkononi! Inanikera sana yani, natamani wangekua wanasema mapema ili nigeuze palepale Airport, lakini wajanja hawakuambii!!”
Swali jingine likawa linahusu njia anayoitumia kusafiri safari za mbali, DJ Khaled alisema >>“….mimi kusafiri natumia basi na nimenunua private bus yangu kurahisisha kazi, yani hata iwe safari ya wapi nitakuja na basi, hata kuja hapa Los Angeles kwa ajili ya hii interview nimekuja na basi, hapa nlipo nina miaka 6 ama 7 sijapanda ndege na wala sina mpango wa kubadilisha msimamo huu”.
Kuhusiana na show za Kimataifa je??>>>“nipo kwenye mpango ambao bado unaendelea wa kununua boti yangu.. yes nipo kwenye mpango wa kufanya hicho kitu kwa sababu niko serious kabisa sitaki kupanda ndege… hata kama ikitokea basi itokee tuu ila asinishawishi mtu kitu chochote kuhusu kupanda ndege…sipendi na ninaogopa!

No comments:

Post a Comment