TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, June 2, 2015

Burundi: waandamanaji wakata tamaa baada ya mkutano wa Dar es Salaam 

Mtoto huyo anaangalia jinsi askari polisi wakiondoa vizuizi viliyowekwa kwenye barabara za mji wa Bujumbura, Mei 30 mwaka 2015.
Mtoto huyo anaangalia jinsi askari polisi wakiondoa vizuizi viliyowekwa kwenye barabara za mji wa Bujumbura, Mei 30 mwaka 2015.
Na RFI
Baada ya mkutano wa marais wa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki uliyofanyika Jumapili Mei 31 jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania, raia katika wilaya za mji wa Bujumbura, nchini Burundi, hasa waandamanaji wamekata tamaa kufauatia uamzi wa marais hao.
Suala muhimu la awamu ya tatu ya Rais Pierre Nkurunziza halikuchukuliwa uamzi katika mkutano huo au hata kujadiliwa na marais hao wa nchi za Afrika Mashariki. Watu wamechukizwa na jambo hilo na wako tayari kuendelea na maandamano.
Katika wilaya za mji wa Bujumbura kunakofanyika maandamano kama Cibitoke na Nyakabiga, raia wamekata tamaa. Lakini pia wamekua na hasira, baada ya mapendekezo yaliyotolewa katika mkutano wa jumuiya ya nchi za Afrika Mashariki.(P.T)
Wakaazi wa wilaya hizo walikua na matumaini kuwa viongozi hao kutoka nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki wangemtaka rais Pierre Nkurunziza kuacha kuwania awamu ya tatu. Suala la kuahirishwa kwa uchaguzi kwa mwezi mmoja na nusu halina mabadiliko yoyote katika msimamo wao.
" Tumekataa tamaa moja kwa moja, kwa sababu hawakusema chochote kuhusu awamu hii ya tatu ya rais Nkurunziza. Marais wa kanda hii hawana uwezo wa kumshawishi Nkurunziza kuacha kuwania awamu ya tatu. Tunahitaji jumuiya ya kimataifa kutusaidia ili tuweze kukabiliana na mgogoro huu ", amesema raia mmoja aliyehojiwa na RFI.
" Hatukua na matumaini makubwa kuhusu mkutano huo. Tuna machungu kutokana na uamzi huo. huo ni usaliti wa moja kwa moja. Tutaendelea kuandamana, tutaendelea na harakati zetu. Lakini ukweli hatimaye utashinda ", wamesema raia wangine wa mji wa Bujumbura.
Serikali ya Burundi imekaribisha mapendekezo ya marais wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuahirisha Uchaguzi kwa angalau mwezi mmoja na nusu ili kukabiliana na hali ya kisiasa nchini humo.
Hata hivyo upinzani unasema umesikitishwa na mapendekezo ya marais hao waliokutana mwishoni mwa juma lililopita jijini Dar es salaam na wameapa kuendelea na maandamano makubwa jijini Bujumbura leo Jumatatu.
Pacifique Nininahazwe kiongozi wa maandamano amesema kuwa wamesikitishwa kuwa viongozi hao wameshindwa kumwambia rais Nkurunziza kutowania urais kwa muhula wa tatu.
Uchaguzi wa wabunge nchini Burundi umepangwa kufanyika tarehe tano mwezi huu, huku ule wa urais ukifanyika tarehe 26.
Itafahamika kwamba rais wa Burundi Pierre Nkurunziza hakushiriki mkutano huo na aliwakilishwa na waziri wake wa mambo ya nje Alain Nyamitwe. Hata rais wa Rwanda Paul Kagame alisusia mkutano huo, akibaini kwamba viongozi wa jumuiya ya Afrika Mashariki wamekua wakipigana chenga kuhusu uamzi mabo unapaswa kuchukuliwa dhidi ya muhula wa tatu wa rais Pierre Nkurunziza.

No comments:

Post a Comment