Burundi: waandamanaji wakata tamaa baada ya mkutano wa Dar es Salaam
Mtoto huyo anaangalia jinsi askari polisi wakiondoa vizuizi viliyowekwa kwenye barabara za mji wa Bujumbura, Mei 30 mwaka 2015.
Na RFI
Baada ya 
mkutano wa marais wa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki uliyofanyika 
Jumapili Mei 31 jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania, raia katika 
wilaya za mji wa Bujumbura, nchini Burundi, hasa waandamanaji wamekata 
tamaa kufauatia uamzi wa marais hao.
Suala 
muhimu la awamu ya tatu ya Rais Pierre Nkurunziza halikuchukuliwa uamzi 
katika mkutano huo au hata kujadiliwa na marais hao wa nchi za Afrika 
Mashariki. Watu wamechukizwa na jambo hilo na wako tayari kuendelea na 
maandamano.
Katika 
wilaya za mji wa Bujumbura kunakofanyika maandamano kama Cibitoke na 
Nyakabiga, raia wamekata tamaa. Lakini pia wamekua na hasira, baada ya 
mapendekezo yaliyotolewa katika mkutano wa jumuiya ya nchi za Afrika 
Mashariki.(P.T)
Wakaazi 
wa wilaya hizo walikua na matumaini kuwa viongozi hao kutoka nchi za 
jumuiya ya Afrika Mashariki wangemtaka rais Pierre Nkurunziza kuacha 
kuwania awamu ya tatu. Suala la kuahirishwa kwa uchaguzi kwa mwezi mmoja
 na nusu halina mabadiliko yoyote katika msimamo wao.
" 
Tumekataa tamaa moja kwa moja, kwa sababu hawakusema chochote kuhusu 
awamu hii ya tatu ya rais Nkurunziza. Marais wa kanda hii hawana uwezo 
wa kumshawishi Nkurunziza kuacha kuwania awamu ya tatu. Tunahitaji 
jumuiya ya kimataifa kutusaidia ili tuweze kukabiliana na mgogoro huu ",
 amesema raia mmoja aliyehojiwa na RFI.
" Hatukua
 na matumaini makubwa kuhusu mkutano huo. Tuna machungu kutokana na 
uamzi huo. huo ni usaliti wa moja kwa moja. Tutaendelea kuandamana, 
tutaendelea na harakati zetu. Lakini ukweli hatimaye utashinda ", 
wamesema raia wangine wa mji wa Bujumbura.
Serikali 
ya Burundi imekaribisha mapendekezo ya marais wa Jumuiya ya Afrika 
Mashariki kuahirisha Uchaguzi kwa angalau mwezi mmoja na nusu ili 
kukabiliana na hali ya kisiasa nchini humo.
Hata 
hivyo upinzani unasema umesikitishwa na mapendekezo ya marais hao 
waliokutana mwishoni mwa juma lililopita jijini Dar es salaam na wameapa
 kuendelea na maandamano makubwa jijini Bujumbura leo Jumatatu.
Pacifique
 Nininahazwe kiongozi wa maandamano amesema kuwa wamesikitishwa kuwa 
viongozi hao wameshindwa kumwambia rais Nkurunziza kutowania urais kwa 
muhula wa tatu.
Uchaguzi wa wabunge nchini Burundi umepangwa kufanyika tarehe tano mwezi huu, huku ule wa urais ukifanyika tarehe 26.
Itafahamika
 kwamba rais wa Burundi Pierre Nkurunziza hakushiriki mkutano huo na 
aliwakilishwa na waziri wake wa mambo ya nje Alain Nyamitwe. Hata rais 
wa Rwanda Paul Kagame alisusia mkutano huo, akibaini kwamba viongozi wa 
jumuiya ya Afrika Mashariki wamekua wakipigana chenga kuhusu uamzi mabo 
unapaswa kuchukuliwa dhidi ya muhula wa tatu wa rais Pierre Nkurunziza.
No comments:
Post a Comment